• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAVUVI ILEMELA KUNUFAIKA NA UZINDUZI WA AKAUNTI YA WAVUVI

Posted on: September 24th, 2019

Wavuvi katika Manispaa Ya Ilemela kupitia Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA) wanatarajiia kupata manufaa makubwa mara baada ya kuzinduliwa kwa akaunti ya wavuvi kupitia bank ya Posta Tanzania.

Manufaa mbalimbali yatakayopatikana kwa wavuvi kupitia akaunti hiyo ni pamoja na kuweza kujiwekea Akiba kwa masharti nafuu kupitia TPB bank Kupata Elimu ya kifedha kupitia wataalam wa benki ya TPB, Shughuli zao zitaweza kurasimishwa na kuweza kuwa na sifa za kupata mikopo kupitia bank hiyo. Pamoja na kuchochea maendeleo ya shuguli za uvuvi katika mzunguko mzima ya uvuvi kwa maana ya wamiliki, wachakataji, mama lishe, wajeshi na wachuuzi wadogo wadogo wa samaki.


Benki ya Posta Tanzania (TPB) na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA) zimeingia mkataba pamoja na kutiliana saini uzinduzi wa akaunti ya wavuvi ambayo itajulikana kwa jina la Wavuvi account.

Zoezi hilo la utiaji saini limeshuhudiwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega katika mwalo wa Igombe uliopo Wilaya ya Ilemela ambapo amewataka wadau hao kuhakikisha wanajiunga na akaunti hiyo ili waweze kupata huduma za kifedha zitakazowawezesha zana za kisasa kwa ajili ya shughuli za uvuvi ambazo zitawafanya kupata malighafi kwa wingi, huku akiupongeza uongozi wa TPB bank kwa kuona umuhimu  wa kuwafikia wavuvi katika kuwaletea maendeleo.


“Niwaombe wavuvi mfungue Wavuvi Akaunti katika Benki ya Posta Tanzania (TPB) itakuwa rahisi kwenu kupata msaada ili muweze kufanya biashara ambapo viwanda sasa vimeanza kufufuliwa upya, nasi tumeagiza kwa sasa samaki wote wanaozalishwa katika viwanda vyetu ni lazima wasafirishwe moja kwa moja kwenda nchi za nje kupitia viwanja vyetu vya ndege badala ya kusafirishwa kwenda nchi zingine kupitia viwanja vya ndege vya nchi jirani.” Amesema Mhe. Ulega

Kwa upande wake Mkurugenzi  Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Bw. Sabasaba Moshingi alisema utiaji saini kati ya benki hiyo na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA), ni muhimu kwa kuwa huduma ya Wavuvi Akaunti itawawezsha wavuvi wengi kuwa na utaratibu wa kutumia huduma za kibenki kwa kuwa kwa sasa wengi wao utumiaji wao wa huduma za kibenki upo chini.


Naye Katibu wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA) Bw. Bakari Kadabi aliwaomba wananchi wote kuungana kutokomeza uvuvi haramu na kuuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali kuongeza mnyororo wa thamani kwa wavuvi na vikundi kujiunga na chama kikuu ambapo mkataba huo na TPB utawawezesha wadau wa sekta ya uvuvi kupata elimu ya fedha na kukopeshwa na benki hiyo kwa ajili ya uendelezaji wa kazi zao.


Zoezi hilo la utiaji saini lilifanyika siku ya tarehe 23.09.2019 huku likishuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Ilemela akiwemo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na wananchi mbalimbali.






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.