• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTENDA HAKI

Posted on: November 21st, 2019

Wajumbe 135 wa mabaraza ya Kata 19 za Manispaa ya Ilemela walioapishwa wametakiwa kutenda haki pamoja na kuwasaidia wananchi kupata  haki zao katika migogoro itakayojitokeza amesema Mhe. Hakimu Amani Nelson Sumari alipomaliza kuwaapisha wajumbe hao.


Hakimu Sumari, ambae ni Kaimu Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilemela, amewataka wajumbe hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufasaha na kuwa ambae hatatekeleza atachukuliwa hatua za kisheria na kuwajibishwa kwani kitendo cha kula kiapo ni wazi kuwa wamejifunga na sheria.


“Hakikisha unatenda haki, unasikiliza mashauri, na unatoa maamuzi bila ya upendeleo”, Alisisitiza


John Paul Wanga, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, nae amewapongeza wajumbe hao kwa kuaminiwa  na kuteuliwa kutoka katika kata zao, na kuwasisitiza kuwa lengo kubwa la kazi yao ni usuluhishi wa migogoro mbalimbali inayowakumba watu katika kata zao ili kuweza kudumisha amani na utulivu ili kuweza kuleta maendeleo.

Pamoja na hayo amesisitiza kuhusu suala la viwango vya tozo na kuwaeleza kuwa kila faini au gharama ambayo mwananchi analipa anatakiwa alipe kwa mfumo wa kielektroniki  na kwa mujibu wa sheria ya fedha ili kuondoa suala la rushwa na kuwa kwa kiongozi atakaekiuka taratibu hizo atachukuliwa hatua za kisheria.


Aidha aliwafafanulia baadhi ya majukumu yao ambayo baadhi yake ikiwa ni kuwa hawana mamlaka ya kusikiliza migogoro ya ardhi iliyopimwa na kama watafanya hivyo watakuwa wamekiuka sheria na maamuzi hayo yatakuwa batili.


Mkurugenzi aliwasisitizia kuhusu suala la kutokuwa na upendeleo wakati wanasikiliza migogoro mbalimbali. “ Tusiamue migogoro kwa upendeleo”, alisisitiza


Nae Mstahiki Meya Mh: Renatus Mulunga aliwasisitiza wajumbe hao kuhusu suala zima la kuhakikisha kuwa wanatenda haki kwa wananchi pamoja na kuepukana na vitendo vya rushwa kwani hakuna mtu ambae yuko juu ya sheria, alisema.

Vilevile Afisa Mipangomiji na ardhi wa Manispaa ya Ilemela, Ndugu Shukurani Kyando nae alipata wasaa wa kuongea na wajumbe hao walioapishwa na kusema kuwa migogoro mingi katika Halmashauri inahusiana na masuala ya ardhi hivyo aliwaelekeza kuwa wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni na sio kwa kufuata maono yao binafsi na kuhakikisha kuwa shauri wanalosikiliza hawana maslahi nayo.

Ndugu Ivan Masao ambae ni Mwenyekiti wa Baraza la ardhi na Nyumba Mwanza aliwapongeza Ilemela kwa kutokuwa na migogoro mingi, aidha aliwaelekeza wajumbe wa mabaraza hayo kuzingatia suala la uwiano wa kijinsia katika kusikiliza migogoro mbalimbali.

Akihitimisha zoezi hilo Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela, Patrick Muhere, aliwahimiza wajumbe hao kwenda kutekeleza majukumu yao kwa ueledi na kwa kuzingatia maadili na miongozo mahsusi ili kujiepusha na vitendo vya rushwa ili kurudisha imani kwa wananchi tunaowahudumiwa na haki itaoneka kutendeka katika jamii.

Mabaraza ya kata ni vyombo vilivyoundwa kwa mujibu wa kifungu cha 3 cha Sheria ya mabaraza ya kata ya mwaka 1985, ambapo kila baraza linajumuisha wajumbe wasiopungua wanne na wasiopungua wanane watakaochaguliwa na kamati ya kata kutoka miongoni mwa majina ya wakazi wa kata yaliorodheshwa kwa kuzingatia taratibu maalum uliowekwa.






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.