• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE 2019 AIPONGEZA ILEMELA UTOAJI WA MIKOPO

Posted on: May 23rd, 2019

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imepongezwa kwa jinsi inavyozingatia matakwa ya Sera ya kuhakikisha inatenga na kutoa mikopo ya asilimia 4 kwa vijana, asilimia 4 kwa wanawake na asilimia 2 kwa walemavu.


Pongezi hizo zimetolewa na kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 Ndugu Mzee Mkongea Ally wakati akikagua shughuli za uzalishaji mali zinazofanywa na kikundi cha Vijana Igombe ikiwa ni muendelezo wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika wilaya ya Ilemela

Mkongea ameisifu na kuipongeza halmashauri hiyo kwa kuona umuhimu wa kutekeleza Sera hiyo ya Serikali inayosaidia vijana kupata mtaji na kujiajiri katika utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo badala ya kujikita katika mambo yasiyofaa ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vya kihalifu


‘.. Nitumie nafasi hii kuipongeza halmashauri ya manispaa ya Ilemela kwa kuona umuhimu wa kutenga fedha kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake  na watu wenye ulemavu  maana zipo halmashauri nchini hazitengi na zile zinazotenga zinatoza riba kitu ambacho ni kinyume na maagizo ya Serikali…’ Alisema


Akimkaribisha kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mheshimiwa Daktari Severine Lalika amemhakikishia kiongozi huyo kuwa wilaya ya Ilemela itaendelea kutekeleza shughuli za maendeleo kwa kushirikiana na wananchi sanjari na kutekeleza maagizo yote yanayotolewa na Serikali.


Nae Mbunge wa jimbo la Ilemela mheshimiwa Daktari Angeline Mabula amemuomba kiongozi huyo kufikisha salamu za shukrani na pongezi kutoka kwa wananchi wa jimbo la Ilemela kwenda kwa mheshimiwa Rais Daktari John Magufuli kufuatia fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya jimbo hilo.

Aidha Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019,Ali Mkongea amekemea halmashauri zinazotoza riba katika utoaji wa mikopo hiyo huku akiwaasa vijana kuhakikisha wanatumia vizuri fedha zinazotolewa kwa kuhakikisha wanazitumia kwa shughuli za uzalishaji mali zitakazosaidia kuwakwamua kiuchumi.

Hadi sasa katika mwaka wa fedha 2018/2019  Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imeshatoa kiasi cha fedha Shilingi za Kitanzania Milioni 244 kwa  vikundi vya wanawake,vijana na walemavu.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "TUUFANYE USAFI KUWA NI TABIA YA KUDUMUA": ANNA MBAO

    May 31, 2025
  • WATAALAM WA MANISPAA YA ILEMELA WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA MFUMO WA MANUNUZI WA UMMA

    May 29, 2025
  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.