Jumla ya kiasi cha Tshs. 78,008,589,777/= zimeidhinishwa na kupitishwa na baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ikiwa ni makisio ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021. Kati ya fedha hizo Tshs. 20,487,197,770/= ni Ruzuku ya miradi ya maendeleo, Tshs.1,952,189,901/= ruzuku ya matumizi ya Kawaida, Tshs. 46,471,289,106/= mishahara na Tshs. 9,097,914,000/= mapato ya ndani.
Akiwasilisha makisio na mpango wa bajeti, kwa niaba ya Mkurugenzi, Mophen Mwakajonga ambae ni mchumi wa Manispaa alisema kuwa, mapato yanayotokana na vyanzo vya ndani yameongezeka kutoka 8,878,387,000.00 (2019/2020) hadi Tshs 9,097,914,000.00 (2020/2021) sawa na ongezeko la asilimia 2.5
Alifafanua kuwa, kati ya mapato ya ndani, kiasi cha Tshs 5,144,096,400/= sawa na asilimia 60 ya mapato zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo 10% ambayo ni sawa na Tshs 857,349,000/= ya uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake, vijana na walemavu.
Ndugu Mophen alivitaja vipaumbele kuwa ni pamoja na ujenzi, afya, elimu msingi na sekondari, ardhi na mipangomiji, utawala, maendeleo ya Jamii, usafishaji na mazingira ,mpango,takwimu na ufuatiliaji, fedha na biashara,mifugo na uvuvi,kilimo na umwagiliaji,ushirika pamoja na nyuki.
Sambamba na uwasilishaji wa mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021, Halmashauri imewasilisha maombi maalumu yenye jumla ya Tsh. 9,000,000,000/= kama ifuatavyo;ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Halmashauri wenye jumla ya Tsh. 2,800,000,000/=, kupatiwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya. Manispaa imeomba kiasi cha Tshs 700,000,000/= kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huu, miradi ya kimkakati ya ujenzi wa standi ya mabasi na maegesho ya msalori Nyamhongolo Tshs 5,500,000,000/=.
Pia Halmashauri imewasilisha maandiko ya miradi 2 yenye thamani ya Tshs. 1,256,032,450.00 ambapo kiasi cha Tshs 983,635,000.00 ni kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa 40 katika shule za sekondari na msingi na kiasi cha Tsh. 272,397,450.00 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati za Lumala na Nyamadoke.
Katika kipindi cha mwaka 2019/2020 Halmashauri ilipanga kukusanya na kupokea jumla ya Tshs 68,063,798,023.00/= kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za Maendeleo na matumizi ya kawaida na hadi kufikia tarehe 31 Desemba, 2019 jumla ya Tshs 29,089,156,182.00 zimekusanywa na kupokelewa kutoka vyanzo mbalimbali hii ni sawa na 43%
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.