• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

Posted on: July 4th, 2025

"Ili uweze kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi tunakutegemea uzingatie vitu vitatu ambavyo ni kuhakikisha unaweka mipango sahihi ya kazi, kuisimamia mipango yako vizuri, kwa kupima na kutekeleza kwa usahihi, na upimaji wa utekelezaji wa mipango yako"

 

Rai hiyo imetolewa na Mwalimu Sylvester Murimi Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari alipokuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela wakati akifunga semina elekezi iliyotolewa kwa walimu wa ajira mpya na tume ya utumishi wa walimu siku ya tarehe 03 Julai, 2025

 

Sambamba na hilo mwalimu Sylvester amewataka walimu hao kujiepusha na kuwa  chanzo cha migogoro sambamba na kuepuka mahusiano mabaya mahala pa kazi baina ya watumishi na wanafunzi kiujumla.

 

Aidha Bi Tabitha D. Bugemwe ambae ni afisa utumishi kutoka manispaa ya Ilemela  akiongea na walimu hao amewaeleza kuwa kazi ya ualimu ni wito, hivyo anatamani kazi hii iendelee kuwa wito ndani yao pia kwasababu tupo kwenye dunia ya utandawazi hivyo kama mwalimu usipokuwa makini kama mwalimu, mzazi na mlezi, hamtaweza kuwafikisha watoto mahali ambapo wanatakiwa kufika.

 

"Ualimu ni wito hivyo naomba mkauishi ndani yenu wito huu wa ualimu kwa kuwa walimu bora, zingatieni sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayotolewa kila wakati katika utendaji wenu wa kazi, kulea na kusimamia vema wanafunzi kwani mwalimu ni mlezi serikali na wazazi wameawaamini na kuwakabidhi watoto muwalee na kuwaelimisha ili kujenga taifa lijalo, Tendeeni haki nafasi mlizopata kwa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi mkiyazingatia haya mtaona kuwa utumishi wa umma ni mzuri na mwepesi " ",alisisitiza Bi Tabitha.

 

Nae Bi Penina Alphonce Katibu msaidizi wa Tume ya Utumishi wa walimu aliwakumbusha walimu hao kuzingatia  masuala ya maadili na nidhamu kwa walimu huku akiwahimiza kuzingatia waraka wa serikali wa mavazi na kuhakikisha wanavaa mavazi ya kiutumishi.

Akishukuru kwa niaba ya wenzake mwalimu Boaz Mwambelwa ambae ameajiriwa hivi karibuni amesema kuwa yeye amekaa miaka tisa bila ajira toka amemaliza chuo, ambapo ameahidi kufanya kazi kwa bidii na ueledi na kuzingatia miiko ya ualimu.

 

Semina hiyo elekezi iliyoratibiwa na tume ya utumishi wa walimu ililenga kuwajengea uwezo walimu juu ya masuala mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo haki na wajibu, maadili na nidhamu, utunzaji wa nyaraka na kumbukumbu, na masuala ya rushwa ambapo jumla ya walimu 134 wa ajira mpya wamepatiwa semina elekezi kati yao walimu 108 ni wa sekondari na 26 ni wa msingi 

 

 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

    July 09, 2025
  • PROF NAGU AMEWATAKA WATUMISHI KADA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    July 08, 2025
  • WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

    July 04, 2025
  • ELIMU YA FEDHA KUWAONGEZEA UFANISI WANUFAIKA WA TASAF

    July 03, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.