• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

"UPANDAJI WA MICHE YA MATUNDA UWE ENDELEVU";DC MKALIPA

Posted on: November 20th, 2025

" Napenda kusisitiza kuwa upandaji wa miche ya matunda uwe endelevu,sambamba na utoaji wa elimu ya lishe kwa vitendo (shamba darasa), pelekeni huduma hii katika shule na zahanati nyingi zaidi ili watoto wetu na jamii kwa ujumla waendelee kujifunza elimu ya lishe kwa vitendo"

 

Rai hii imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe. Amiri Mkalipa Tarehe 20/11/2025 katika maadhimisho ya siku ya kitaifa yaliyofanyika katika mtaa wa Imalang’ombe kata ya Sangabuye huku akibainisha dhumuni la maadhimisho hayo kuwa ni kuongeza uelewa katika jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa jamii.

 

Aidha Mhe Mkalipa amewaagiza wataalamu wa lishe wilayani Ilemela kuweka mkazo zaidi kwenye kutoa elimu ya lishe katika maeneo yote ya Ilemela ili kuweza kuwa na watoto wenye afya bora kwani kufanya hivi kutasaidia kuondokana na maradhi yatokanayo na ukosefu wa lishe bora.

 

Sambamba na maelekezo hayo Mhe. Mkalipa pia ametoa wito kwa kina baba kutimiza wajibu wao katika malezi ya watoto kwani kuna maradhi kama vile udumavu na utapiamlo wakati mwingine husababishwa na wazazi kutokutimiza wajibu wao. 

 

Kwa upande wake Bi. Ummy Wayayu, mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, amesema kuwa kufuatia elimu ya masuala mbalimbali ya lishe na afya iliyotolewa katika maadhimisho hayo anaamini kuwa jamii itakwenda kuyafanyia kazi kikamilifu na itakwenda kubadilika katika mtazamo  chanya.

 

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli na afua za lishe katika Manispaa ya Ilemela, Afisa Lishe Bi. Pili Kasim amesema miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kupungua kwa hali ya utapiamlo kutoka asilimia 2.9 hadi asilimia 2.0 na pia halmashauri imefanikiwa kuanzisha kilimo cha mazao kwenye shule za msingi na sekondari 22, bustani 17 za mbogamboga pamoja na vituo vitatu vinavyotoa huduma za afya lengo ikiwa ni kuwasaidia wanafunzi na jamii kujifunza kwa vitendo elimu ya lishe.

 

“Nitoe wito kwa jamii kuhakikisha inafuata mtindo bora wa maisha pamoja na kuzingatia ulaji unaofaa ili kuepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.” Alisema Bi. Pili

 

Akizungumza Ndg. Jeremia Samweli Daniel mkazi  wa mtaa wa Imalang’ombe amewaasa wazazi na walezi kuwahudumia watoto wao na kuwapatia huduma ya lishe bora ili wakue katika hali nzuri. Huku Bi. Semeni Peter mkazi wa mtaa wa Imalang’ombe ameishukuru serikali kwa kuwapelekea maadhimisho hayo na kutoa wito kwa kina baba na kina mama kushiriki kikamilifu katika matukio kama hayo.

 

Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu isemayo,"Afya ni mtaji wako;Zinagtia unachokula" yameenda sambamba na utoaji wa huduma za utoaji wa matone ya vitamin A na dawa za minyoo kwa watoto chini ya miaka 5, upimaji wa HIV, homa ya Ini, Saratani ya matiti, huduma za macho, masikio na kinywa pamoja na shughuli mbalimbali za  utoaji wa elimu ya lishe,ulaji unaofaa kwa mama mjamzito na mama anayenyonyesha, umuhimu wa kutumia vyakula vilivyoongezwa virutubisho, jiko darasa, ugawaji wa unga wa lishe sambamba na upandaji wa miti ya matunda.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • ORODHA MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO WALIOTEULIWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2025 JIMBO LA ILEMELA October 20, 2025
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA VYUMBA VYA BIASHARA October 16, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "UPANDAJI WA MICHE YA MATUNDA UWE ENDELEVU";DC MKALIPA

    November 20, 2025
  • WATAHINIWA 7912 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2025 MANISPAA YA ILEMELA

    November 17, 2025
  • DC MKALIPA AHIMIZA VIKAO NA WAZAZI JUU YA MASUALA YA LISHE MASHULENI

    November 17, 2025
  • WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO 2879 WAAPISHWA,WAMEASWA KUZINGATIA SHERIA KANUNI NA MIONGOZO

    October 26, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.