• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

Posted on: July 9th, 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia wataalam wake wa mifugo wameendelea na uchanjaji wa kuku ikiwa ni awamu ya kwanza ya zoezi la uchanjaji wa mifugo, na utekelezaji wa mkakati wa serikali wa kupunguza na kutokomeza vifo vya mifugo ambapo wafugaji wa kuku wameendelea kunufaika na chanjo hiyo ya kideri, ndui na mafua makali ya kuku inayoendelea kutolewa katika kata zao. 

 

Wafugaji hao wa kuku katika nyakati tofauti wameishukuru serikali kwa kuleta chanjo hizi kwani kupitia ufugaji wamekuwa wakiongeza kipato chao huku  wakitarajia kuwa kupitia chanjo hii kuku wataepukana na magonjwa. 

 

“Huko nyuma nilikuwa nawatibu kuku wangu kwa njia ya kienyeji, walisumbuliwa sana na magonjwa na wengine walikufa lakini sasa hivi natarajia mifugo yangu itakuwa na afya njema kupitia hizi chanjo",Bw. Philipo Opati mkazi wa  kata ya kahama 

 

Naye kijana Yakobo Leonard, mtoto wa mfugaji wa kuku katika kata ya kahama amesema kuwa ufugaji wa kuku unawasaidia kuongeza kipato,  chakula na kumuendeleza kielimu hivyo ameishukuru serikali kwa kutekeleza zoezi la utoaji wa chanjo kwani litasaidia afya ya mifugo yao kuimarika na pato la familia litakua.

 

Bi. Recho Thomas kamalambo mkazi wa kata ya Buswelu ambaye pia ni mfugaji wa kuku ameeleza kuwa kuku wake wamekuwa wakisumbuliwa na magonjwa mbali mbali  na wengi wamefariki kwa kukosa maelekezo sahihi ila kwa sasa atazingatia maelekezo ya wataalam  katika kuhakikisha mifugo yake inaepukana na mgonjwa.

 

Kwa upande wake  Dkt. Nelson Rugemukamu, Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela amebainisha kuwa tangu kuanza kwa zoezi hilo tarehe 03.07.2025 hadi sasa, kata 11 kati ya 19 za Manispaa ya Ilemela zimeshafikiwa na zoezi hili

 

“Hadi sasa kata 11 kati ya 19 zilizopo katika halmashauri yetu zimeshafikiwa na zoezi la utoaji wa chanjo ambalo litahitimishwa tarehe 14 Julai, 2025 hivyo nawasihi wafugaji muendelee kutoa ushirikiano kwa wataalam ili zoezi liweze kukamilika kwa mafanikio” Alisitiza Dkt. Nelson

 

 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

    July 09, 2025
  • PROF NAGU AMEWATAKA WATUMISHI KADA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    July 08, 2025
  • WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

    July 04, 2025
  • ELIMU YA FEDHA KUWAONGEZEA UFANISI WANUFAIKA WA TASAF

    July 03, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.