• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Zaidi ya milioni 60 kuchochea miradi ya maendeleo jimbo la Ilemela

Posted on: May 2nd, 2022

Kiasi cha shilingi milioni sitini na laki tatu na elfu tisini na sita kutoka katika fedha za mfuko wa jimbo zimetumika kwaajili ya kuchochea shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya jimbo la Ilemela .



Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza walimu wa shule za sekondari kwa kupata matokeo mazuri kitaaluma Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amesema kuwa jimbo lake limepokea kiasi hicho cha fedha kwaajili ya shughuli za kimaendeleo ambapo shilingi milioni 30 ilitumika kwaajili ya kununua gari aina ya Mitsubish Delicia yenye usajili namba SM 14564 itakayotumika kwaajili ya kusafirishia wataalam wanaofanya kazi katika maeneo yasiyofikika kiurahisi au shughuli za misiba inapojitokeza katika jamii huku kiasi cha shilingi milioni 27 ikitumika kwaajili ya ununuzi wa samani za ofisi kwa walimu wa shule 27 za Sekondari za Serikali, milioni 4.5 ikitumika kwaajili ya ununuzi wa seti tatu za kompyuta kwa shule 3 za Sekondari zilizofanya vizuri ikiwemo Bwiru wavulana, Kilimani na Nyasaka, milioni 9 ikitumika kutengeneza madawati 120 ambayo yatagawanywa kwa shule 4 za msingi zenye uhaba mkubwa na milioni 13 na elfu 50 zikitumika kwaajili ya ununuzi wa mifuko 580 ya saruji itakayozalisha tofali 23,200 ambayo yatagawanywa kwa ajili ya kujenga maboma ya ofisi za mitaa17
‘.. Lengo langu ni kuleta motisha ya ushindani kielimu, tutagawa japo kwa uwakilishi kidogo tulichopata mbele ya wenye duka kwa maana ya wenye Ilani ya uchaguzi chama cha mapinduzi ili wajue katika kata zao tumefanya nini ..’ Alisema


Aidha Mhe Dkt Mabula amemshukuru Rais Mhe Samia Suluhu Hasan kwa fedha za maendeleo alizozitoa katika jimbo lake ambapo ndani ya mwaka mmoja zaidi ya bilioni 30 zimekwisha tolewa huku akiwataka wananchi wa jimbo hilo kumpongeza na kumuombea kiongozi huyo ambae pia ni mlezi wa wilaya ya Ilemela

Kwa upande wake mstahiki meya wa manispaa ya Ilemela Mhe Renatus Mulunga mbali na kumpongeza mbunge huyo ameahidi kuisimamia manispaa hiyo kupitia baraza lake la madiwani katika kuhakikisha fedha zinazoletwa na Serikali zinatumika kama zilivyokusudiwa ili miradi iweze kukamilika kwa ubora unaotakiwa na kwa wakati sahihi

 Nae kaimu mkurugenzi wa manispaa hiyo Ndugu Sitta Singibala amemshukuru mbunge huyo pamoja na kuahidi ushirikiano katika kutekeleza miradi ya maendeleo ndani ya manispaa hiyo itakayosaidia kupunguza changamoto mbalimbali kwa wananchi

Wasinyo Werema ni mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Bwiru wavulana kwa sasa ambae amemshukuru mbunge wa jimbo la Ilemela pamoja na kumpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya katika kusukuma gurudumu la maendeleo huku akitaja baadhi ya manufaa aliyoyapata akiwa mkuu wa shule mbili kwa nyakati tofauti kutoka kwa mbunge huyo ikiwemo taulo za kike alizozitoa shule ya sekondari Sangabuye yeye akiwa mwalimu mkuu na futari kwa wanafunzi wa shule ya Bwiru yeye pia akiwa mwalimu mkuu.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.