• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAZAZI NA WALEZI WAMETAKIWA KUZINGATIA LISHE KWA VIJANA BALEHE

Posted on: October 30th, 2023


Wazazi na walezi wametakiwa kuzingatia mlo kamili wenye virutubisho vyote vinavyohitajika katika makuzi na afya ya binadamu hasa kwa vijana wanaokua

Rai hiyo imetolewa na mwakilishi wa mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela  ambae pia ni afisa elimu msingi takwimu Mwalimu Johanes  John wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya lishe duniani kiwilaya yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Buswelu yakipambwa na kauli mbiu ya ‘ Lishe bora kwa vijana balehe, Chachu ya mafanikio yao’ ambapo amewataka wazazi na walimu kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalam wa lishe na afya katika aina ya vyakula kwaajili ya kuukinga mwili dhidi ya magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza  ili vijana waweze kukua vizuri na kulitumikia vyema taifa lao

‘.. Tafiti mbalimbali zimefanyika na kutokana na tafiti hizo imeonekana watu tunapata chakula lakini hatupati chakula bora kwaajili ya manufaa ya miili yetu na akili yetu na kama hatuli vizuri lazima tuelimishane namna bora ya aina ya chakula, Baada ya siku ya leo tusikilize ushauri wa wataalam wetu na rika hili la vijana balehe ndio rika kusudiwa sababu rika hili linataka akili nzuri iliyotulia hivyo lazima ale vizuri ..’ Alisema

Aidha Mwalimu Johanes  ameongeza kuwa ni wajibu wa wazazi na walezi kwenda kusimamia utaratibu wa lishe kwa vijana wao pindi wanapokuwa majumbani na kuasa kutopuuzwa kwa elimu ya lishe inayotolewa na wataalam

Kwa upande wake mratibu wa lishe manispaa ya Ilemela Bi Pili Kasimu amefafanua kuwa kwa robo ya kwanza ya Julai-Septemba 2023/2024 vijana waliopatiwa elimu ya ulaji unaofaa na kufanyiwa tathimini ya hali ya lishe ni 390 ambapo vijana 111 sawa na asilimia 28.5 walikuwa na hali nzuri ya lishe,  vijana 179 sawa na silimia 45.9 walikuwa na uzito uliozidi, vijana 61 sawa na asilimia 15.6 walikuwa na uzito uliokithiri pia vijana 39 sawa na asilimia 10 walikuwa na uzito pungufu pamoja na kukabiliwa na changamoto za vijana kutozingatia muda wa kula chakula na kujikita katika anasa mbalimbali ikiwemo kuangalia luninga, ushiriki mdogo wa kina baba katika malezi na makuzi ya vijana balehe, vijana kupendelea vyakula visivyofaa na kuchangia magonjwa yasiyoambukiza  ikiwemo chips na soda

Getruda Cosmas ni mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Kaselya ambapo yeye ameshukuru kwa maadhimisho hayo kufanyika katika shule yao pamoja na kupongeza zoezi la upimaji hali za lishe lililofanywa na wataalam wa manispaa ya Ilemela katika kilele cha maadhimisho hayo pamoja na kuomba zoezi hilo liwe endelevu badala ya kusubiria shughuli za maadhimisho za kila mwaka

Wilaya ya Ilemela inajivunia mafanikio ya kupungua kwa kiwango cha utapiamlo ambapo kwa mwaka 2021/2022 utapiamlo ulikuwa asilimia 3 na sasa mwaka 2022/2023 utapiamlo ni sawa na asilimia 2.9

 


Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.