• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WATUMISHI IDARA YA AFYA WAASWA KUWAJIBIKA IPASAVYO

Posted on: November 10th, 2023

Watumishi wa idara ya afya wa Manispaa ya Ilemela wameaswa kuwajibika ipasavyo kila mmoja kwa nafasi yake kwa kufanya kazi kwa weledi na bidii ili kuleta matokeo chanya katika huduma mbalimbali za afya zinazotolewa kwenye vituo vya kutolea huduma hizo.


Hayo yamesemwa na mwakilishi wa mganga mkuu wa mkoa Bi.Ester Maliki ambaye pia ni katibu wa afya mkoa wa Mwanza wakati alipohudhuria kikao kazi cha idara hiyo katika ukumbi wa manispaa ya Ilemela kilichohokuwa na malengo ya kufanya tathimini ya utekelezaji wa huduma za afya zilizotolewa kuanzia Januari hadi Septemba 2023 sambamba na kujadili changamoto na kuzipatia ufumbuzi na kuboresha huduma hizo.


“Kila mtu awajibike kwa nafasi yake,mvae umiliki wa kila kinachofanyika kwenye maeneo yenu,usimamizi wa miradi mbalimbali ,ukusanyaji na usimamizi wa mapato kwenye vituo vyetu ni jukumu la wote kikubwa ni kugawana majukumu ili mambo yaende kwa mpangilio mzuri.” Amesema Bi.Ester


Pamoja na hilo Bi.Ester ametoa pongezi kwa kazi nzuri inayoendelea katika idara ya afya Manispaa ya Ilemela akaongeza kusema kuwa kazi hii ya huduma za afya ni wito hivyo wazidi kuipenda na kuifanya kwa bidii zaidi ili huduma ziwe bora zaidi.


Nae Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilemela Dkt.Samson Marwa amesisitiza suala la wahudumu wa afya kutoa elimu za masuala ya kiafya kwa jamii hasa hasa masuala ya lishe bora ambayo ndio inamjenga mtu kuwa imara kiakili .


“Jamii inapaswa kufahamu mchanganyo wa makundi matano ya vyakula,wanga,protini,mbogamboga,matunda na sukari na mafuta bila kusahau maji kwa kuzingatia vipimo sahihi vyenye tija sio kula tu mladi kushiba.” Amesema Dkt.Marwa


Sambamba na hayo Dkt.Marwa ametoa wito kwa wahudumu wa afya katika vituo vyote vya kutolea huduma ndani ya manispaa ya Ilemela kuweka utaratibu wa kutoa elimu ya usafi wa mazingira ili kuepuka magonjwa ya kuhara na kipindupindu ambayo yameanza kutokea kwa mikoa jirani.


“Kuchukua tahadhari ya kipindupindu ni muhimu na sisi kama wataalam wa afya tunawajibika kuelimisha jamii juu ya majanga hayo hasa nyakati hizi za mvua.”


Bi.Emila Msangi ni katibu wa afya Manispaa ya Ilemela yeye amesisitiza suala la ukusanyaji wa mapato kwa watumishi vituoni na kufanya kazi kwa umoja kwa manufaa ya wote.


“Kadri mnavyokusanya ndivyo mtakavyokuwa huru kutumia kwa matumizi yenu yenye tija katika maboresho ya utoaji huduma vituoni,ipo haja ya kubuni mbinu zaidi za kuwavutia wateja wetu.”  Amesema Bi.Emila


Taarifa mbalimbali za kiafya kama vile hali ya lishe,Malaria,kifua kikuu,huduma za ustawi wa jamii zimewasilishwa na kujadiliwa lengo ikiwa ni kuboresha utoaji wa huduma.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.