• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WATOTO 131,828 KUCHANJWA CHANJO YA MATONE YA POLIO AWAMU YA NNE

Posted on: November 30th, 2022

Manispaa ya Ilemela kupitia idara ya Afya imelenga kutoa chanjo ya matone ya polio kwa watoto 131,828 wenye umri chini ya miaka 5.


Mhe Hassan Masala Mkuu wa Wilaya ya Ilemela ambae ni Mwenyekiti wa kamati ya afya ya Msingi Wilaya ya Ilemela, amewataka wataalam wa afya kuwaelimisha wananchi umuhimu wa chanjo ya matone ya polio ili kuweza kuondokana na dhana potofu juu ya chanjo hii.


Ametoa wito huo wakati akiongoza kikao cha kamati ya Afya ya msingi kilicholenga kuongeza uelewa kwa wanajamii juu ya chanjo kwa ajili ya kumlinda mtoto dhidi ya polio kwani ni gonjwa usio na tiba hivyo chanjo ni kwa ajili ya kuimarisha kinga.


Pamoja na wito huo Mhe Masala amewapongeza wataalam wa afya kwa namna wanavyojitoa katika kuhudumia wananchi pamoja na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha lengo lililowekwa na Serikali la kuwafikia watoto wote wanaotakiwa kupata chanjo

‘.. Niwatie Ari mtakapoendelea na zoezi hili tutawapa ushirikiano na tupo tayari kushirikiana nanyi kutatua changamoto zozote zitakazojitokeza kwani tunachotaka ni wananchi wetu wawe salama na sisi tupo kwa ajili ya kulinda usalama wao ..’ Alisema


Mratibu wa chanjo Ndugu Shamte Almasi, ametoa wito kwa wazazi na walezi wasikatae chanjo kwani madhara ya ugonjwa wa polio ni makubwa ambayo yanaweza kupelekea kifo lakini pia watoto kupata ulemavu wa kudumu wa  mikono na miguu.


Pamoja na hayo  amewataka kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuwapatia chanjo watoto hao  ili lengo la kutokomeza ugonjwa huu wa polio liweze kufikiwa sambamba na hilo ameomba wazazi au walezi kuacha maelekezo juu ya kampeni hii ili kurahisisha zoezi hili.


Kampeni ya chanjo ya polio itafanyika kwa siku nne kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 4 mwezi wa kumi na mbili 2022 katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya serikali na binafsi vinavyopatikana katika Manispaa ya Ilemela, nyumba kwa nyumba na maeneo yenye mikusanyiko ya watu kama vile sokoni. Sambamba na uchanjaji huduma zingine zitatolewa ikiwemo elimu ya chanjo na kuimarisha huduma za chanjo katika vituo vya kutolea chanjo.


Ikumbukwe Polio ni ugonjwa usiokuwa na tiba na unaosababishwa na virusi vya polio, ugonjwa huu unasababisha kupooza na hatimaye kifo.








Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.