• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WATAALAM WATAKIWA KUTOA ELIMU UMUHIMU WA BIMA YA AFYA KWA JAMII

Posted on: October 9th, 2024

Wataalam wa idara ya afya Manispaa ya Ilemela wameshauriwa kuwafikia wananchi kwa ajili ya kuwapa elimu ya umuhimu wa bima ya afya ili waweze kuepukana na gharama kubwa wakati wa matibabu.

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe. Dkt .Angeline Mabula wakati wa mkutano wake wa hadhara katika viwanja vya Kangae 'B' kata ya Nyakato ambapo amesema kuwa ipo haja kwa wananchi kuelewa kwa kina juu ya bima ili iwe rahisi kukata bima hizo .

"..Ni ngumu sana hawa wananchi kukata bima kama hawana uelewa wa kutosha kuwa bima ina faida gani kwao, bahati nzuri hata sisi wawakilishi wao tumeshapitisha sheria ya bima lakini hili halipaswi kuishia katani tu au wilayani, mtenge muda muwafikie wananchi .."Alisema

Aidha Dkt.Mabula amewataka wananchi wa kata hiyo kuwa wavumilivu kutokana na kero ya changamoto za barabara kwa kuwa Manispaa ya Ilemela imeweka mkakati wa ununuzi wa ununuzi wa mitambo ya ujenzi wa barabara ili kurekebisha barabara za mitaa

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Ndugu Jeremiah Lugembe mbali na kumpongeza mbunge huyo kwa kazi nzuri anazozifanya amemuhakikishia mbunge huyo kuwa kazi ya uelimishaji juu ya masuala mbalimbali ya afya inaendelea na kwamba mitaa yote itafikiwa.

Lugembe amekiri kutambua makundi mbalimbali yanayopatikana ndani ya manispaa hiyo ikiwemo bodaboda ,wazee na kuahidi ushirikiano na kuwataka kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi .

Lilian Chiguma ni mwakilishi wa mganga mkuu wa Wilaya ya Ilemela ambapo amesema kuwa serikali inaendelea na juhudi katika kuboresha sekta ya afya hivyo kuwaasa wananchi kuiunga mkono na kukata  bima za afya ili kuepuka gharama wakati wa matibabu .

Silvanus Manija na Nusra Yahya Ramadhan ni wananchi wa mtaa wa Kangae 'B' ambapo licha ya kumpongeza mbunge wao na Serikali kwa kazi kubwa iliyofanyika wamelalamikia ubovu wa barabara za mtaa huo na kero ya ukosefu wa maji  safi na salama katika maeneo yao.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.