• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ELIMU YA MABADILIKO YA TABIA NCHI YATOLEWA KWA MAAFISA UGANI KILIMO MANISPAA YA ILEMELA

Posted on: September 29th, 2025

Kuelekea msimu wa kilimo mwaka 2025/2026 Manispaa ya Ilemela kupitia Divisheni ya kilimo,Mifugo na Uvuvi leo tarehe 29/09/2025 imeendesha mafunzo kwa maafisa ugani kilimo wai ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. 

 

Mafunzo hayo yamelenga kuwaelimisha maafisa ugani pamoja na wadau wa kilimo juu ya mabadiliko ya tabia nchi na uwepo wa mvua za vuli za wastani  hadi chini ya wastani kwa kipindi cha mwezi Oktoba - Disemba 2025 ili waweze kuwasaidia na kuwashauri wakulima waweze kulima mazao ya muda mfupi na yanayoweza kuhimili ukame pia watumie mbegu zilizo na ubora na zenye uzalishaji mkubwa.

 

"Lengo letu ni utabiri huu wa hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi yatuelekeze namna gani tutawasaidia wakulima kujua mazao gani walime na kwa wakati gani wapande ili kukabiliana na mabadiliko haya ya tabia nchi  na waweze kunufaika na kilimo chao” James Wembe Afisa kilimo.

 

Naye ndugu Agustino Nduganda Meneja TMA kanda ya Ziwa alitoa mwelekeo wa mvua za vuli za mwaka huu 2025 kuwa zinatarajia kuanza kunyesha wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Oktoba na zitakua mvua za wastani hadi chini ya wastani tofauti na ilivyozoeleka. Kwa kawaida wastani wa mvua katika miezi ya Oktoba-Desemba kwa wilaya ya Ilemela ni kati ya milimita 360 hadi 410.

 

Bi. Grace Minja Afisa kilimo kata ya Kiseke kwa niaba ya washiriki amewashukuru wawezeshaji wa mafunzo kwani  yamewawezesha kuweza kwenda kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi kuelekea msimu huu wa kilimo na kuwashauri wakulima wafate kanuni bora za kilimo na kuweza kupata uzalishaji wenye tija.

 

Mafunzo hayo ni hatua muhimu katika juhudi za Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuimarisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi, huku yakilenga kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii wananchi.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • ORODHA MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO WALIOTEULIWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2025 JIMBO LA ILEMELA October 20, 2025
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA VYUMBA VYA BIASHARA October 16, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • ILEMELA YAANZA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI 2026/2027

    November 25, 2025
  • "UPANDAJI WA MICHE YA MATUNDA UWE ENDELEVU";DC MKALIPA

    November 20, 2025
  • WATAHINIWA 7912 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2025 MANISPAA YA ILEMELA

    November 17, 2025
  • DC MKALIPA AHIMIZA VIKAO NA WAZAZI JUU YA MASUALA YA LISHE MASHULENI

    November 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.