• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WASICHANA 2898 KUNUFAIKA NA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

Posted on: April 25th, 2018

 

Zaidi ya wasichana wasiopungua 2898 katika Manispaa ya Ilemela wanatarajia kunufaika na chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi ambayo inaendelea kutolewa katika maadhimisho ya wiki ya chanjo ambayo huadhimishwa nchi nzima, bara na  visiwani.

Akizindua rasmi chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi na maadhimisho ya wiki ya chanjo kitaifa kwa Wilaya ya Ilemela, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela John Wanga ambae alimwakilisha mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe Khadija Nyembo, amesema kuwa lengo la maadhimisho ya wiki ya chanjo ni kuhakikisha kuwa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano ambao hawajakamilisha chanjo wanapata kwani chanjo ni haki ya kila mtoto.


 

Aidha alisema kuwa katika wiki hii ya chanjo,  Wilaya ya Ilemela  inatarajia kuchanja wasichana wasiopungua 2898 dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi.

 


“Katika wiki hii ya maadhimisho ya chanjo manispaa ya Ilemela tunatarajia kuchanja wasichana wasiopungua 2898 dhidi ya saratani ya mlago wa kizazi”, alisema

 

Aliongeza kuwa, sambamba na kutoa chanjo ya saratani, manispaa pia itatoa chanjo mpya ya kuzuia ugonjwa wa polio ambayo itatolewa kwa njia ya sindano na sio matone kama hapo awali.

 


Akihutubia wananchi, Mkurugenzi John alizitaja dalili za ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi pamoja na kuzitaja sababu zinazochangia kuenea kwa ugonjwa huo ikiwemo kujamiiana katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi, kuwa na ndoa za mitala, kuzaa watoto wengi pamoja na uvutaji wa sigara huku shirika la afya ulimwenguni WHO likikadiria kuwa zaidi ya wagonjwa wapya 50,000 wa saratani ya mlango wa kizazi hubainika kila mwaka nchini Tanzania.



Nae kaimu mganga mkuu wa manispaa ya Ilemela Bi Maria Kapinga amewatoa hofu wazazi juu ya chanjo hiyo ikiwa ni pamoja na kuwataka kuwaruhusu watoto wao kuhudhuria vituo vya kutolea huduma ili waweze kuchanjwa.

Kwa upande wake mwakilishi wa shirika la afya (WHO) aliyehudhuria uzinduzi huo, Ndugu Arlen Galimo ameipongeza halmashauri kwa  uzinduzi huo wa utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi amewaasa wahudumu wa afya wa manispaa hiyo kutimiza wajibu wao kwa kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na magonjwa hayo.
Nchini Tanzania, maadhimisho ya wiki ya chanjo kwa watoto hufanyika kila mwaka wiki ya mwisho ya mwezi wa nne ambapo kwa mwaka huu maadhimisho haya katika Wilaya ya  Ilemela yameambatana na uzinduzi wa chanjo mbili mpya ambazo ni chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi na chanjo ya sindano ya kuzuia ugonjwa wa polio ikiwa na  kauli mbiu ya ‘JAMII ILIYOPATA CHANJO NI JAMII YENYE AFYA, TIMIZA WAJIBU WAKO’

 




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.