• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANAWAKE WA ILEMELA WAJITOA KUSAIDIA WAHITAJI

Posted on: March 4th, 2025

Kuelekea siku ya wanawake duniani Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia idara ya maendeleo ya jamii imeunganisha makundi mbalimbali ya  wanawake  wa Ilemela ikiwemo wadau kutoka mashirika ya siyo ya kiserikali, wafanyabiashara,wajasiriamali ,watumishi wa umma na wasio na shughuli rasmi katika tendo la kutoa kwa ajili ya wahitaji.

Wanawake hao walitembelea kata tatu za Kayenze ,Sangabuye na Bugogwa ambapo lengo kuu ilikuwa ni kuwatembelea watoto wanaoishi mazingira  magumu ,watoto wanaojilea wenyewe ,watoto yatima na kutoa misaada ya hali na mali ikiwa ni sehemu ya kuwaonyesha upendo na kuwatia moyo kuishi bila kukataa tamaa na kutumia changamoto zao kama fursa.

“..Unaweza ukawa unapitia maisha magumu sana lakini hali hiyo isikusababishe kushindwa kusoma au kupoteza matumaini,wapo viongozi wengi wakuu wa nchi hii waliozaliwa na kukulia mazingira magumu sana.Tupo hapa kwa upendo msijisikie wanyonge ninyi ni watoto wetu..”  Amesema Neema Majura Mratibu wa dawati la jenda Ilemela .

Sophia Nshushi ni mdau kutoka shirika lisilo la kiserikali la Teen Corridor Organization  yeye anasema mtoto anapokuwa tumboni ni wa kwako akishazaliwa ni mtoto wa wote hivyo ushiriki wao katika matendo ya huruma kama hayo ni kawaida yao huku akiwasisitiza watoto wanaojilea wenyewe kuendelea kuwa na nguvu ya kupambana na vishawishi mbalimbali katika hatua zao za ukuaji kimwili na kihisia na kuhakikisha wanatimiza malengo waliojiwekea.

Zulfa Cornel (13) ni mwanafunzi kutoka shule ya msingi Bezi anatoa shukrani  kwa kwa kina mama hao kwa misaada iliyotolewa huku akiahidi kusoma kwa bidii kutimiza ndoto zake za kuwa daktari.

Mwalimu Mashaka Edward Msiba ambae ni mlezi wa wanafunzi waishio kwenye mazingira magumu katika shule ya msingi Kisundi amewaombea kila lililo jema kina mama wote walioshiriki zoezi hilo la utoaji kwa wahitaji.

“..Mungu awabariki sana kina mama kwa kijitoa kwenu ,mmetoa muda wenu, pesa zenu kwa ajili ya hawa watoto.Mungu awazidishie pale mlipotoa..”

Jumla ya watoto 60 wamenufaika na msaada huo ambapo vitu vilivyotolewa ni mchele,sukari,mafuta ya kupikia,sabuni za unga ,sabuni vipande na za maji,mafuta ya kupaka ,dawa za meno na mahitaji madogo madogo ya shule kama madaftari na kalamu.

  

 

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.