• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wananfunzi wajengewa uwezo kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji

Posted on: March 9th, 2021

Na Paschalia George

Wanafunzi wa shule za sekondari katika Manispaa  ya Ilemela wamejengewa uwezo wa kutambua na kuripoti vitendo vya unyanyasaji, ukatili,uvutaji bangi na madawa ya kulevya na kujiepusha na mimba katika umri mdogo ili kujenga taifa lililo bora lenye wataalam wenye weledi na mlengo chanya kimaendeleo


Akizindua mpango huo wa kutoa elimu ya kujitambua na kupambana na vitendo vya ukatili mashuleni, Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amesema kuwa ni wajibu wa jamii nzima ya Ilemela kila mmoja kwa nafasi yake kuelimisha wanafunzi juu ya mambo mbalilmbali yanayowahusu katika makuzi yao sambamba na kutoa pongezi kwa uongozi wa jeshi la polisi na Halmshauri ya manispaa ya Ilemela kwa kuungana katika kubuni jambo hili lenye manufaa kwa wanafunzi na jamii nzima ya Ilemela.


Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Dkt Mabula ametoa rai kwa wanafunzi kujiepusha na matukio yote yasio na faida kwao huku akisisitiza wanafunzi hao kujiepusha na uvutaji bangi na matumizi ya madawa ya kulevya,mimba mashuleni ,vitendo vya unyanyasaji na ukatili.

“Wanangu wa kike nataka mjiepushe na lifti hasahasa za bodaboda, msipende vya bure. Kila mmoja afahamu kwa nini yuko hapa,wazazi wamewaleta shuleni msome jukumu lenu kubwa ni hilo. Muwe wepesi kutoa taarifa za matukio yasiyo ya kawaida punde yanapojitokeza”


Nae Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Wilaya ya Ilemela Afande Shamira Kasimu Mkomwa amezungumzia kwa undani juu ya madhara ya madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na mtumiaji kutengwa na jamii kwa sababu ya kuwa na mambo ya hovyo hovyo yasiyo na tija sambamba na madhara ya kiuchumi ambayo yanasababisha jamii kuwa duni katika masuala ya kimaendeleo.


“  Hatuitaji taifa lenye wataalam wavuta bangi wala madawa ya kulevya, wanyanyasaji au viongozi wenye matukio ya ajabu ajabu yasiyofaa kwa maadili yetu ya kitanzania tunataka taifa lenye uhai na watu timamu. Mtoe taarifa haraka kwa jeshi la polisi punde mnapoona moja ya matukio hayo kwani jeshi la polisi lipo kwa ajili ya kulinda raia na mali zao.”amesema

Wanafunzi hao pia wamenufaika na elimu ya usalama barabarani iliyotolewa na kaimu afisa usalama barabarani wilaya ya Ilemela afande Hosiana Mushi kwa kuwasisitiza juu ya umakini na kufuata sheria pindi wanapotumia barabara.

Aidha Afisa elimu sekondari ndugu Emmanuel Malima amewaasa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani ndilo jambo pekee litakaloonyesha nuru katika maisha yao.


“Wasichana chipsi ni chakula cha kawaida tu msitoe utu wenu kwa ajili ya chipsi,wavulana pia achaneni na magenge yasiyofaa kuja shule kukaa kwenye mawe au maporini amkeni wanangu muone umuhimu wa nyie kuwepo hapa”amesema

Mwanafunzi, Joseph Elias Masanja ameshukuru kwa elimu iliyotolewa kwani itawasaidia katika kubaini na kuripoti matukio yote yasiyofaa katika jamii tofauti na hapo awali ambapo ilikuwa ngumu kwao kubaini aina za matukio ya ukatili na hatua za kuchukua.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.