• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI WATAKIWA KUZINGATIA MPANGO KABAMBE WA MATUMIZI YA ARDHI

Posted on: October 8th, 2024

Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza  wametakiwa kuzingatia mpango kabambe (master plan) wa matumizi ya ardhi ili kuepuka ujenzi holela na kushusha thamani ya ardhi wanazomiliki .

Rai hiyo imetolewa na mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe. Dkt. Angeline Mabula wakati wa zoezi la kusikiliza na kuzipatia ufumbuzi kero na changamoto za ardhi kupitia kliniki ya ardhi iliyofanyika katika ukumbi wa Winterfell kata ya Nyasaka ambapo amefafanua kuwa Serikali imetumia gharama kubwa kuandaa mpango huo kabambe wa matumizi ya ardhi unaolenga kutoa muongozo wa namna bora ya kupanga mji kulingana na matumizi yake .

“.. Mkoa wetu wa Mwanza kwa bahati nzuri unao mpango kabambe wa matumizi ya ardhi, mpango ambao umefafanua kila eneo limepangwa kwa matumizi gani, unakuta mtu eneo zima amejenga fremu tu na jirani yake fremu utafikiri hakuna uwekezaji mwengine.Tukiufuata mpango kabambe umeelekeza wazi wapi tunapaswa kufanya nini na kama hauwezi basi muingie mikataba na wawekezaji wengine ili kuongezea thamani maeneo yetu ..” Alisema

Aidha Mhe. Dkt. Mabula amezitaka mamlaka za ardhi mkoa wa Mwanza na manispaa ya Ilemela kuzingatia maelekezo ya kamati ya bunge juu ya kurejesha eneo la shule ya sekondari Kisenga kata ya Kiseke na kumlipa fidia mwananchi aliyetwaliwa eneo lake au kumpatia eneo jingine ili shule hiyo iweze kuwa na eneo la kutosha kukidhi mahitaji yake na kutekeleza maelekezo ya kamati hiyo.

Kwa upande wake kamishina wa ardhi msaidizi mkoa wa Mwanza Bi. Happines Mtutwa amesema jumla ya hati miliki 95 za maeneo tofauti ndani ya Manispaa ya Ilemela zimetolewa kwa wananchi huku akipongeza zoezi la kliniki ya ardhi linaloendelea kuwa limekuwa la mafanikio makubwa kwa kupunguza kero nyingi za ardhi Ilemela.


“..tumetumia mbinu za kuweka kambi maeneo mbalimbali kwa lengo la kuwafikia wananchi wengi zaidi kusikiliza na kutatua kero zao za ardhi huku tukiwaelimisha juu ulipaji kodi za ardhi na elimu ya master plan ili wajue mgawanyo wa matumizi ya ardhi ..” 

Nae diwani wa kata ya Nyasaka Mhe. Abdulrahman Simba amempongeza mbunge huyo kwa kazi nzuri anayoifanya ndani ya jimbo lake.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.