• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wananchi wa Manispaa ya Ilemela watakiwa kugharamia zoezi la urasimishaji MakaziI

Posted on: March 2nd, 2017

WANANCHI WA MANISPAA YA ILEMELA WATAKIWA KUGHARAMIA ZOEZI LA URASIMISHAJI MAKAZI Wananchi wa Manispaa ya Ilemela wametakiwa kugharamia zoezi la urasimishaji wa makazi yao ili kusaidia upangaji wa mji sambamba na kuepuka ujenzi holela usiofuata sheria na taratibu za matumizi ya ardhi Hayo yamebainishwa na Afisa Mipango Miji wa Manispaa Ilemela Ndugu Kennedy Chigulu alipokuwa Mtaa wa Ibanda kata ya Kirumba baada ya Kamati ya Mipango Miji ya Manispaa hiyo kufanya Ziara yake ya kawaida ya kukagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na Manispaa hiyo Akizungumza katika ziara hiyo Bwana Chigulu amesema kuwa kwa kawaida Serikali haigharamii zoezi la urasimishaji isipokuwa wananchi wenyewe ndiyo wanagharamia hivyo kazi ya Serikali ni kusimamia zoezi hilo na kuhakikisha taratibu zote za kitaalamu zinafuatwa na kuzingatiwa Hayo yamekuja kufuatia mgogoro wa mipaka uliojitokeza baina ya kata mbili za Kirumba na Kitangiri wakati wa zoezi la urasimishaji linaloendelea katika eneo hilo la Ibanda ambapo amewatahadharisha kuwa suala la kimipangomiji halina mipaka ya kiutawala kwani mchoro unapotoka huwa hauoneshi mipaka ya kiutawala hivyo kwa viongozi na wananchi wanapaswa kuelewa hivyo huku akitaka kukutanishwa kwa pande hizo kutoa elimu ya upimaji shirikishi Kufuatia mgogoro huo Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Diwani wa Kata Kirumba Mheshimiwa Alex Ngusa amewataka wananchi kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha maeneo yote stahiki yanapimwa na kurasimishwa sambamba na kuchangia huku akitanabaisha kuwa Kamati yake haitavumilia mtu yeyote mwenye lengo la kukwamisha zoezi hilo na kuwataka viongozi kukaa na wananchi wao kufanikisha zoezi hilo ‘… Wenyeviti wa Mitaa na Kamati zenu fanyeni vikao na wananchi wa muhakikishe wanachangia zoezi la upimaji na urasimishaji wa makazi yao, Hii ni kwa faida yetu na Sisi hatutamvumilia mtu yeyote atakaekwamisha zoezi hili… Aidha Kamati imewataka Viongozi na wataalam wa Manispaa kuwachukulia hatua wananchi wote wanaofanya shughuli za uharibifu wa mazingira na kuhamasisha upandaji miti ili kutunza mazingira yao kwa faida ya vizazi vijavyo na vya sasa Wajumbe wa kamati hii pamoja watalaam wa Manispaa ya Ilemela walitembelea maeneo mbalimbali yakiwemo ya mradi wa maji Igombe, ukaguzi wa mazingira kiwanda cha nguo Mwatex, ujenzi wa barabara ya mawe Kawekamo, ujenzi wa daraja Cassanova, na mabadiliko ya matumizi ya ardhi Nyamanoro

Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.