• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI WA ILEMELA WATAKIWA KUTII SHERIA BILA SHURUTI

Posted on: June 29th, 2017

WANANCHI WA ILEMELA  WATAKIWA KUTII SHERIA BILA SHURUTI



Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Ndugu John Wanga amewataka wananchi kutii sheria bila shuruti kwa kufuata taratibu ili kuweza kuyafikia malengo ya serikali katika kuwaletea maendeleo.


Hayo aliyasema wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Shibula juu ya utatuzi wa mgogoro wa ardhi unaohusisha eneo la jeshi la wananchi kikosi cha anga, eneo la uwanja wa ndege na wananchi hao ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makaazi Daktari Angeline Mabula alilolitoa mapema wiki hii baada ya kufanya kikao na wananchi hao.


“Siku hizi kumekuwepo na vizazi visivyofuata haki na wajibu na hiki ndicho kinachofanya sheria zivunjwe, Niwaombe sana unapodai haki ni lazima utimize wajibu wako tusiwe kama wale watu wanaotumwa na wazungu kusababisha vurugu ili waweze kulipwa pesa, Nawaomba tena ndugu zangu tufate sheria na taratibu, Tusikubali kutumika na viongozi wachache wenye maslahi yao binafsi kwa kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani pasipo sababu ya msingi”, Alisema.



Aidha Mkurugenzi Wanga amewataka viongozi wa maeneo yanayoguswa na mgogoro huo kuacha mara moja kushawishi wananchi kugomea utekelezaji wa shughuli za maendeleo na kushinikiza vitendo vya kihalifu kwa kuwa kufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria na kuwa Serikali haitamvumilia mtu yeyote kwa ridhaa yake ama kushawishiwa atakaejihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani huku akiwaasa juu ya kudai haki zao kwa utaratibu unaokubali na usioleta madhara kwa wengine .

Kwa upande wake afisa mipango miji wa Manispaa ya Ilemela Anna Mhamba amewahakikishia wananchi hao kuwa siku ya jumatatu atashirikiana na wataalamu wengine kufika eneo la tukio kubaini mipaka inayolalamikiwa na pande zote na mwisho kuwasilisha taarifa hiyo kwa ngazi husika ili iweze kufanya maamuzi sahihi yenye maslahi mapana kwa pande zote yakizingatia haki bila uonevu kwa yeyote.



Nae Diwani wa kata ya Shibula Mheshimiwa Swila Dede kwa niaba ya wananchi ameushukuru Uongozi wa Ilemela kwa namna inavyolishughulikia suala hilo huku akiahidi kutoa ushirikiano katika kufanikisha zoezi hilo la utatuzi wa suluhu ya mipaka ya pande hizo.







Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.