• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI WA ILEMELA WANAVYONUFAIKA NA TASAF

Posted on: November 13th, 2024

Serikali kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF), inalenga kuongeza fursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa na kulinda maslahi ya watoto wao, kwa kuhakikisha watoto wenye umri wa kupelekwa kliniki wanapelekwa na wanafunzi wanapatiwa mahitaji ya shule

 

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ni miongoni mwa halmashauri ambazo zimeendelea kunufaika na mpango huu wa kunusuru kaya maskini kwa kupokea fedha ambazo hutolewa kwa walengwa wa kaya maskini pia kwa ajili ya kujenga miundombinu mbalimbali katika sekta za afya, elimu na miundombinu ya barabara.

 

Katika kipindi cha robo ya kwanza Julai hadi Septemba mwaka wa fedha 2024/2025, Manispaa ya Ilemela imepokea jumla ya fedha kiasi cha shilingi milioni 800.86 (Tshs 800,864,599), ikiwa ni fedha kwa ajili ya walengwa wa kaya maskini na fedha kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za kijamii

 

Kati ya fedha hizo shilingi milioni 216.07 (Tshs. 216,076,310) ni fedha kwa ajili ya malipo ya walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini kwa kaya 3447 zinazonufaika na mpango huo.

 

Kwa upande wa uboreshaji huduma za kijamii na kiuchumi shilingi milioni 584.78 (Tshs 584, 788,289.97) zimepokelewa katika robo ya kwanza 2024/2025 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata za Kayenze na Kiseke. Kwa upande wa kata ya Kiseke shilingi milioni 101.23 zimepokelewa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na shilingi milioni 483.55 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya afya na elimu katika kata ya kayenze.

 

Sikujua Maluba Migisi ni mnufaika wa mpango huu wa kunusuru kaya maskini kutoka mtaa wa Butuja kata ya Ilemela, yeye anaishukuru TASAF kwani kupitia mpango huu ameweza kuwanunulia Watoto wake mahitaji ya shule lakini si hivyo tu fedha hiyo imemuwezesha kufungua biashara ndogo ambapo faida ikipatikana humsaidia kukidhi mahitaji ya nyumbani na watoto shuleni huku akiwakumbusha wakina mama wenzake kuwa wanapopata fedha hizi wazitumie kwenye biashara kukuza mtaji wao na matumizi ya nyumbani.

 

Bwana Sinja Jumanne mkazi wa mtaa wa PPF kata ya Kiseke, anasema kuwa kabla ya kujiunga na mpango wa TASAF Maisha yake yalikuwa chini sana lakini sasa maisha yameboreka kwani kupitia fedha hizo ameweza kukodi mashamba ambapo kupitia kilimo anapata kipato cha kukidhi mahitaji yake na ya familia yake.

 

Betia Nyajoro mkazi wa mtaa wa Isenga kata ya Kiseke anasema awali alikuwa anaweza kukosa hata fedha ya kununua mahitaji ya shule ya Watoto wake, lakini kupitia fedha hiyo ya TASAF alianzisha biashara ndogo ambapo hadi sasa mtaji wake umeenda unakua, amewashari wanufaika wenzake kuwa pindi wapatapo fedha hii wasiendekeze pombe bali watumie fedha hizo kuanzisha biashara ndogo ndogo ili kukuza kipato chao

 

“Fedha hii ukiitumia kwa malengo inakuinua, tusiidharau kuwa ni fedha ndogo inatusaidia sasa hivi hali niliyo nayo mimi sio kama awali kabla sijajiunga na mpango huu wa TASAF” alisema Bi Betia.

 

Nao wananchi wa mtaa wa Bezi kata ya Kayenze katika nyakati tofauti wameishukuru serikali kwani kupitia fedha za TASAF sasa kisiwa cha Bezi kinaenda kuboresha huduma za afya kwa wananchi wake, ambapo kiasi cha shilingi milioni 202.46 zimepokelewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje na ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa afya.

 

Leonard Robert ni mratibu wa TASAF Manispaa ya Ilemela, ametoa rai kwa walengwa wa mpango huu kwa kuwataka walengwa hao kujiunga kwenye vikundi vya walengwa ili kujijengea utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza ili watakapohitimu katika mpango waweze kujitegemea kiuchumi.

 

Mwisho amewataka walengwa hao kutumia ruzuku wanazopokea katika kuanzisha au kuendeleza biashara ndogondogo, ufugaji, kuboresha makazi ,kilimo cha bustani na kuhudumia familia zao.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.