• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI WA ILEMELA WAITIKIA KAMPENI YA UJENZI WA MADARASA

Posted on: August 3rd, 2022

Wananchi kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela wameitikia wito wa kampeni ya ujenzi wa madarasa inayoendelea katika Manispaaa hii, hilo limedhihirishwa baada ya wananchi hao kujitokeza katika zoezi la uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi wa Shule za Msingi mpya katika kata za Kahama, Shibula na Buswelu ambalo linaongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe Hasan Masala.


Wananchi hao wamesema wamelazimika kujitokeza katika zoezi hili la uchimbaji msingi kwa ajili ya uanzishwaji wa shule za msingi mpya katika kata hizo kufuatia changamoto mbalimbali ambazo watoto wao wamekuwa wakizipata.



Wakizitaja changamoto hizo kwa nyakati tofauti wamesema kuwa changamoto ya watoto kutembea umbali mrefu kufika shuleni, msongamano wa wanafunzi katika madarasa, walimu kuwa na mazingira magumu ya, walimu kushindwa kufuatilia wanafunzi vizuri darasani ni baadhi ya changamoto zilizopelekea wananchi wa Ilemela kuitikia wito wa kushiriki kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika kata mbalimbali.


"Ujenzi wa shule hizi mpya utawawezesha walimu kuwafuatilia wanafunzi darasani kwa ukaribu kutokana na kuondokana na msongamano wa wanafunzi, itaondoa utoro shuleni, utaongeza ufanisi katika ufundishaji pamoja na kuboresha mazingira ya kujifunza na kujifunzia pamoja na kuboresha taaluma katika kata hizo". walisema



Nae Mwalimu Rehema Suleyman wa kata ya Kahama amewataka wanajamii kujitokeza katika mazoezi haya kwani ni faida ya watoto wao na kuonyesha kuwa ipo shida na uhitaji wa miundombinu ya shule ikiwa ni pamoja kutoa moyo kwa serikali inayopambana kila siku ambayo inahakikisha inapatikana miundombinu katika sekta ya elimu



Akishiriki zoezi la uchimbaji wa misingi katika kata hizo, Mhe. Hasan Masala Mkuu wa Wilaya ya Ilemela akiwa na Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na Mkurugenzi na wataalam wa Manispaa ya Ilemela, amebainisha malengo ya zoezi hilo ni kupunguza au kuondoa kabisa changamoto ya uhaba ya vyumba vya madarasa katika wilaya ya Ilemela hali inayopelekea wanafunzi kukosa maeneo ya kujifunzia.


“Kiwilaya tuna upungufu wa vyumba vya madarasa takriban 1200, hivyo tumeonelea ni lazima sisi wenyewe tupambane kuhakikisha tunapunguza uhaba wa vyumba vya madarasa na ikiwezekana tunaondoa kabisa changamoto hii”, amesema Masala



 Aliongeza kwa kuiomba jamii kutoa ushirikiano wa kutosha huku akiwasisitiza kuwa wajenge maboma na Halmashauri itamalizia kwa kuezeka, na kuweka madawati katika shule hizo mpya huku akiwapongeza kwa utayari wao.



Mhandisi Modest Apolinary Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela amewapongeza wananchi kwa jitihada zao za kushiriki ujenzi wa miradi ya maendeleo,na kuwaahidi kuwa mara baada ya maboma hayo  kukamilika halmashauri itawajibika na suala zima la kukamilisha majengo hayo.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.