• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Wananchi wa Ilemela waendelea kunufaika na TASAF awamu ya tatu

Posted on: August 12th, 2021

Wananchi wa Manispaa ya Ilemela wameendelea kunufaika na mpango wa taifa wa kunusuru kaya maskini awamu ya tatu (TASAF III) kipindi cha pili, ambapo jumla ya kiasi cha Shilingi Milioni 107,112,000 zimelipwa kwa walengwa 2262 walio katika mpango huo katika mitaa 100 ya Ilemela.

Akizungumza na walengwa wa TASAF wa kata ya Buswelu wakati wa utoaji wa mafunzo ya matumizi bora ya pesa hizo, mratibu wa TASAF Manispaa ya Ilemela ndugu Frank Ngitaoh amesema kuwa ni wajibu wa kila mlengwa kutumia pesa zake vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa.


“Ni utaratibu wetu kila mara tunapotoa pesa hizi kutoa elimu kwa walengwa kubuni miradi midogomidogo itakayokuwa chachu ya kukuza vipato vyao kwa kasi ndogo lakini miradi itoe matokeo na kuonyesha ukuaji wao katika kujinasua na hali duni ya kiuchumi”, Alisema


Aidha alisema kuwa TASAF III imetambua changamoto za upokeaji pesa mkononi ikiwa ni pamoja na kufanya matumizi nje ya mpango wakati walengwa wanaporudi majumbani hivyo kuanzisha utaratibu wa kulipa pesa kwa njia ya benki badala ya kupewa pesa mkononi.


Halikadhalika alisisitiza matumizi bora ya pesa hizi kwa kujiunga na utaratibu wa mfuko uliopo sasa wa kufanya malipo kwa njia ya mtandao kupitia simu ,mawakala na benki kwani njia hii ni salama zaidi kwa vile inampa fursa mtumiaji kupanga na kuamua kwa utulivu zaidi kabla ya kushika pesa.


Kwa upande wake Sophia William Shabushi (70) wa mtaa wa Ibaya kata ya Shibula ambae ni miongoni wa walengwa ameishukuru serikali kwa mpango huu, kwani umempa pesa angalau kuweza  kuanzisha miradi midogo midogo ya kumuwezesha kujikimu kiuchumi.


“Sasa hivi nina kibanda cha kuuza mbogamboga na matunda pale nyumbani ninapoishi,kwa siku sikosi elfu mbili kiasi kinachoniwezesha kumudu mahitaji madogomadogo kwangu na wajukuu zangu ikiwa ni pamoja na chakula .Nashukuru sana mpango wa TASAF kwani kweli ni mkombozi wetu” alisema


Hadi sasa Wilaya ya Ilemela imefanikiwa kusajiri kaya 1081 zinazoendelea kupata huduma za kifedha mtandaoni na zoezi la usajili likiwa bado linaendelea.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.