• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI ILEMELA WATAKIWA KUFUATA MAELEKEZO YA WATAALAM WA AFYA KUHUSIANA NA KORONA

Posted on: April 23rd, 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia kamati yake ya Huduma,afya na elimu imefanya ziara maalum kwa kutoa elimu juu ya ugonjwa wa Korona unaosababishwa na virus vya Covid-19 kwa kupita maeneo ya masoko na stendi.

Wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa kamati Mhe.Sarah Ng’hwani ambaye pia ni Diwani wa kata ya Buswelu ameongoza timu hiyo inayoundwa na waheshimiwa madiwani na wataalam mbalimbali wa Manispaa  kwa ajenda moja kubwa ya kupambana na Korona.


Akizungumza katika soko la Buswelu Mhe.Sarah amewataka wananchi wa Ilemela kuwa makini kusikiliza na kufuata maelekezo ya wataalam wa afya juu ya namna ya kuepuka na kujilinda na Korona.Sambamba na hayo Mhe.Ng’hwani amewataka wananchi wanaofanyia shughuli zao maeneo ya msongamano kama masokoni na stendi kukaa angalau mita moja kutoka kwa mtu hadi mtu kama njia mojawapo ya kupunguza uwezekano wa maambukizi kusambaa kwa kasi.


“Ugonjwa huu ni kweli sio mzaha ,wananchi tuchukue tahadhari, kuvaa barakoa sasa ni lazima”amesema.

Kamati hii pia ilifika katika soko la samaki la kimataifa Kirumba maarufu kama Mwaloni na kuongea na wananchi waliokuwepo sokoni.


“Soko hili ni la kimataifa tunapokea wageni kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi hivyo ni lazima kuchukua hatua thabiti katika kujilinda na korona tulikuwa tunaisikia nchi za nje lakini sasa hivi tunayo nchini mwetu sio masihara jamani tunawe mikono mara kwa mara kadri tuwezavyo.


Tukishindwa kufata maelekezo ya kitaalam hapa tutakufa wote na soko hili litafungwa hatutakuwa na shughuli za kutuingizia kipato. Embu tujifikirie maisha yatakuwaje” Amesema Muhasibu wa mapato wa Halmashauri ndugu Andrew Ndaba.


Ziara ya kamati hiyo iliungwa mkono na Umoja wa vijana wa Chama cha  Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Ilemela kwa kugawa sabuni za maji za kunawia mikono zaidi ya lita 200 katika maeneo ya mikusanyiko ambapo kamati imepita kutoa elimu. Soko la samaki Kirumba wamepewa lita 50,soko la matunda Kirumba lita 50, Soko la Buzuruga lita 50,stendi ya mabasi Buzuruga lita 50 na soko la Nyakato lita 25.


Akizungumza wakati wa kukabidhi sabuni hizo Katibu muenezi wa UVCCM wilaya ya Ilemela Denis Kengela Kankono amesema kama vijana wa CCM wameguswa na janga hili lakini pia kitendo hicho ni katika jitihada za kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli katika mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Korona unaotesa taifa na ulimwengu mzima kwa sasa.


“Katika masuala muhimu ya kijamii kama haya tunaweka itikadi zetu zote pembeni,itikadi za kisiasa ,kidini ,ukabila nk hazina nafasi kwetu.Tunawajali na kuwapenda wananchi wetu ndo maana tunajali usalama wenu kwanza.Tunaomba wadau wengine mbalimbali wajitokeze kwa wingi katika kupambana na ugonjwa huu wa Korona.

Akitoa shukrani kwa kamati na UVCCM Mwenyekiti wa umoja wa wakala wa mabasi wa stendi ya Buzuruga ndugu Jacob Nyamatare amesema “Tunashukuru kwa kujali kwenu na kuja kutoa elimu na kutupa sabuni hizi katika kupambana na janga la Korona ila tunazidi kuwaalika tena na tena kwa ajili ya elimu isiyokuwa na mwisho kwani hapa stendi watu ni wabishi mno na hata hivyo tunapokea wageni na watu wapya kila siku”.


Aidha mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Ilemela Bi.Pili Kassimu ameeleza kwa kina dalili za ugonjwa wa Korona ambazo ni homa,kikohozi,kubanwa mbavu na kupumua kwa shida,vidonda kooni,kuumwa kichwa na mwili kuchoka.


“Mnapoona dalili hata moja wahi kituo cha afya kupata huduma.Mkumbuke tunaweza kujikinga na Korona kwa kufunika mdomo na pua wakati wa kukohoa,kuepuka kusalimiana kwa kushikana mikono,kuepuka misongamano,kusafisha mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni.Vipo vingi vya kufahamu tusikilize vyombo vya habari pia na kupenda kusoma mabango maeneo yetu ya kazi.”amesema Bi.Pili.

Akihitimisha ziara hiyo katika eneo la soko la Nyakato Mhe.Ng’hwani amewataka watendaji wa kata na viongozi wa ngazi mbalimbali wilayani Ilemela kuwachukulia hatua wazazi wanaoruhusu watoto wao kuzurura hovyo mitaani kwa kuwatoza faini na kuwaripoti katika ngazi zingine za juu pindi wanapokaidi amri na utaratibu uliowekwa na serikali.


Watoto kufunga shule ni moja ya njia ya kuwakinga na kuwaepusha na maambukizi, lengo la serikali kufunga shule ni pamoja na kutetea uhai wa watoto hawa kwa kuwaepusha na msongamano ambayo ndio njia rahisi ya maambukizi kusambaa kwa haraka.Tunataka watoto wabaki nyumbani ”alihitimisha








Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.