• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANAMICHEZO ILEMELA WATAKIWA KUWA NA NIDHAMU

Posted on: July 28th, 2022

Wanamichezo ambao ni wanafunzi kutoka shule za sekondari Ilemela waliochaguliwa kuunda timu ya UMISETTA ngazi ya wilaya wametakiwa kuhakikisha wanakuwa na nidhamu pamoja na kusikiliza maelekezo ya viongozi wao watakapokuwa katika kambi ili timu hiyo iweze kurudi na ushindi wa ngazi ya mkoa.


Rai hiyo imetolewa na afisa elimu sekondari wa Manispaa ya Ilemela Mwalimu Sylvester Mrimi wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya wavulana Bwiru sekondari yakikutanisha timu kutoka kanda nne za Buswelu, Pasiansi, Bugogwa na Bwiru.

Pamoja na hayo wanamichezo hao wametakiwa kuhakikisha wanakuwa sehemu ya wananchi watakaoshiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi ili kuisaidia Serikali kupata takwimu sahihi kwa ajili ya mipango ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi wengine kuhesabiwa.



“Mwezi Agosti 23 tutakuwa na tukio la Sensa ya watu na makazi, Mimi nitahesabiwa, Nashauri na wana michezo washiriki kuhesabiwa ili Serikali yetu iweze kupanga mipango ya maendeleo yake”. Alisema


Kwa upande wake Mwalimu Kizito Bahati akizungumza kwa niaba ya afisa michezo wa Manispaa ya Ilemela ametoa ombi kwa vilabu vya michezo na shule za michezo vinavyopatikana mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla kusajili wachezaji wanaoibuliwa katika mashindano mbalimbali yanayofanyika ndani ya wilaya


Bi Rosemary Mkama, meneja wa benki ya NMB tawi la Ilemela amesema kuwa benki yake itaendelea kushirikiana na Serikali haswa wilaya ya Ilemela katika kufanikisha shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo michezo huku akiwaalika wanamichezo hao kujitokeza na kunufaika na huduma zinazotolewa na benki hiyo.

Nae mwanafunzi Salome John kutoka shule ya Sekondari Bugogwa mbali na kushukuru kwa timu yake kuibuka kuwa mshindi wa jumla ameongeza kuwa mafanikio waliyoyapata yametokana na timu yao kuwa na maandalizi ya kukutosha, kushirikiana, kusikiliza maelekezo ya mwalimu na kujituma huku akiahidi kufanya vizuri zaidi katika ngazi ya mkoa na kurudi na ushindi.


Mashindano hayo ya UMISETA yamehusisha michezo ya mpira wa miguu, mpira wa mikono, riadha, mpira wa pete, mpira wa wavu na kipekee kwa mwaka huu kumekuwepo na kipengele cha mziki wa singeli ambapo timu ya kanda ya Bugogwa imeibuka mshindi wa kipengele hicho kipya cha singeli pamoja na kutwaa ubingwa wa jumla kuwa mshindi wa kwanza na kutwaa vikombe kumi ikifuatiwa na timu ya kanda ya Buswelu, nafasi ya tatu ikienda kwa Pasiansi na ya nne ikienda kwa kanda ya Bwiru.


Announcements

  • TANGAZO KUHUSU VIWANGO VYA TOZO KATIKA STENDI MPYA YA NYAMHONGOLO August 15, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU STENDI YA NYAMHONGOLO August 12, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA July 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA August 11, 2022
  • View All

Latest News

  • KUANZA KWA STENDI MPYA YA MABASI YA NYAMHONGOLO- WANANCHI WAPONGEZA JITIHADA ZA SERIKALI YA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN

    August 16, 2022
  • UMAKINI NA UADILIFU WASISITIZWA KWA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA MAUDHUI NA TEHAMA ILEMELA

    August 15, 2022
  • ELIMU YA LISHE NA NJIA BORA ZA UNYONYESHAJI YATOLEWA KWA WAKINAMAMA ILEMELA

    August 11, 2022
  • TASAF YAENDELEA KUNUFAISHA KAYA ZA ILEMELA

    August 10, 2022
  • View All

Video

UZINDUZI WA MAJENGO MAWILI YA MAMA NA MTOTO NA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KWA UJENZI WODI YA WAZAZI
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.