• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE WATAKIWA KUWA MFANO BORA WA KUIGWA

Posted on: October 20th, 2022

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela , Mhandisi Modest Apolinary amewataka wanafunzi kidato cha nne kuhakikisha wanakuwa mfano bora wa kuigwa na wenye nidhamu mara baada ya kuhitimu elimu yao ya kidato cha nne

Mhandisi Modest ametoa rai hiyo  wakati wa hafla ya mahafali ya 82 ya shule ya sekondari ya wavulana Bwiru yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo Oktoba 20, ikiwa ni takriban wiki tatu kuelekea mtihani wa kidato cha nne 2022

‘.. Niwaombe vijana mnaotoka hapa leo mnaingia mtaani nendeni mkawe mfano bora, mkawe na nidhamu  msiende kuwa vibaka mtaani, mkawe wazalishaji wakati mkisubiri kuendelea na shule ..’ Alisema


Aidha amewataka wazazi kuendelea kuwalea watoto wao katika maadili yanayofaa mara baada ya kuhitimu mtihani wa kidato cha nne ili kujenga jamii yenye maadili na nidhamu.


Pamoja na hayo Mhandisi Apolinary amekemea vitendo vya utoro mashuleni huku akizitaka bodi za shule na walimu kuchukua hatua dhidi ya vitendo hivyo na kushuka kwa nidhamu huku akisistiza kuwa elimu ya msingi mpaka kidato cha sita inatolewa bure na Serikali chini ya Rais Mhe Samia Suluhu Hasan, Na manispaa yake ikisaidia watoto zaidi ya hamsini walioshindwa kujigharamia huduma za kawaida hivyo hakuna sababu ya mwanafunzi kushindwa kwenda shule

Kwa upande wake makamu mkuu wa shule ya sekondari  Bwiru wavulana Mwalimu Daniel  Ibrahim Kitambara amesema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1920 ikitoa elimu ya msingi na mwaka 1938 ilipanuliwa na kuanza kupokea kidato cha kwanza na kuongeza kuwa kitaaluma imekuwa ikifanya vizuri mwaka hadi mwaka huku lengo kuu likiwa ni kuondoa sifuri kabisa licha ya kukabiliwa na changamoto za upungufu wa mabweni mawili, upungufu wa vitabu vya ufundi na ukarabati wa nyumba za walimu


Philipo Marco Busungu ni miongoni mwa wanafunzi wanaohitimu elimu ya kidato cha nne shule ya sekondari Bwiru wavulana ambapo amewashukuru walimu wake kwa maandalizi mazuri huku akiahidi kufanya vizuri katika mtihani wake wa mwisho sanjari na kuwaomba wanafunzi wanaobaki kuendelea kuzingatia masomo na nidhamu


Sajda Halfan ni miongoni mwa wazazi wenye watoto wanaohitimu ambapo yeye amewapongeza kwa kufikia hatua hiyo pamoja na kuwataka kuendelea kuishi kwa nidhamu


Mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022 unatarajiwa kuanza tarehe 14/11/2022na kukamilika tarehe 01/12/2022 ambapo jumla ya wananfunzi 6905 kutoka katika shule za Manispaa ya Ilemela wanatarajia kufanya mtihani huo kati yao wavulana ni 3376 na wasichana ni 3529

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.