• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WALENGWA WA TASAF WAASWA KUJITENGA NA VITENDO VYA UKATILI

Posted on: March 25th, 2024

Wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF wametakiwa kujitenga na vitendo vya kikatili na unyanyasaji katika ngazi ya kaya ili fedha wanazohawilishiwa ziweze kuleta tija na manufaa.

Rai hiyo imetolewa na afisa ustawi wa kata ya Nyamanoro ambae pia ndie mwezeshaji wa mpango huo katika kituo cha ofisi ya kata ya Kawekamo Bi. Deograsia Lubugo wakati wa zoezi la utoaji wa elimu (Community Session) kwa wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF ambapo amewataka wanufaika kutumia fedha zinazotolewa na mpango huo kwaajili ya shughuli za uzalishaji mali, kujikwamua kiuchumi, mahitaji ya shule, afya badala ya kutumia fedha hizo kunywea pombe na vitendo vyengine visivyofaa vinavyoweza kuchochea ukatili na unyanyasaji katika ngazi ya familia

‘.. Asitokee mtu akatumia fedha hizi kwaajili ya kununulia pombe, ukalewa ukaanza kumpiga mkeo, mumeo au watoto, Tumieni fedha hizi kwaajili ya shughuli za uzalishaji mali, mkifanya hivyo mtakuwa mbali na vitendo vyovyote vya kikatili vinavyoweza kufanyika ..’ Alisema

Aidha Bi Lubugo ameongeza kuwa kiasi cha jumla ya shilingi  2,571,121 kimehawilishwa katika mitaa miwili ya Pasiansi mashariki A na Pasiansi mashariki B iliyopo ndani ya kata anayoisimamia huku akishauri walengwa wanaopokea fedha taslimu mkononi kujitahidi kuhamia katika mfumo wa kupokea kidigitali kwa njia ya benki au simu ya mkononi

Bi Peruce Nkuru  ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Pasiansi mashariki ‘A’ kata ya Kawekamo ambapo amewasisitiza wanufaika wa mpango huo katika mtaa wake kuhakikisha wanatumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa badala ya kununulia nguo za sikukuu na kunywea pombe hasa kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za Pasaka na Eid

Nae Bi Mariam Mohamed ni miongoni mwa wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF kutoka mtaa wa Pasiansi Mashariki ‘A’ ambapo amefafanua kuwa kupitia mradi wa TASAF ameweza kupata fedha zinazomsaidia kuwekeza katika biashara yake ya ufugaji wa kuku na bata hivyo kumudu gharama za maisha ya kila siku pamoja na kuwasomesha watoto na wajukuu zake sanjari na kupata uhakika wa huduma za afya kwa kaya yake.

Jumla ya kiasi cha shilingi milioni 243.5 zimetolewa kwa kaya 5,383 ndani ya manispaa ya Ilemela ikiwa ni malipo ya kipindi cha Novemba – Desemba,2023 kwa mkupuo mmoja.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.