• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI WATAKIWA KUJIANDAA NA UKOMO WA RUZUKU

Posted on: February 3rd, 2025

Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) ndani ya manispaa ya Ilemela wametakiwa kuanza kujiandaa na ukomo wa ruzuku zilizokuwa zinatolewa na mpango huo.


Hayo yamebainishwa na mwezeshaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF kata ya Nyamanoro Ndugu Mbwana Rashid Lunga wakati akizungumza na walengwa hao kabla ya kuanza kwa zoezi la uhawilishaji fedha ambapo amesema kuwa walengwa walioingia kwenye mpango kuanzia mwaka 2021 watatakiwa kuwa wamefuzu katika mpango itakapofika mwezi Septemba, 2025 hivyo kuwaasa kujiandaa kisaikolojia, kimipango na kimkakati 

 

'.. Tujiandae na tuwe na hizi habari kuwa itafika hatua tutafuzu katika mpango huu wa TASAF, Na itakapofika Septemba 30 mwaka huu ndio itakuwa mwisho wa ruzuku kwa walengwa walioandikishwa kuanzia mwaka 2021 mpaka viongozi wetu wa mitaa watakapotupatia taarifa nyengine mpya zitakazolewa na mpango ..' Alisema

 

Aidha Ndugu Mbwana amewataka wanufaika wa mpango huo kuzingatia matumizi bora ya nishati kama sera ya nchi inavyotaka ili kuimarika kiuchumi pamoja na kulinda afya zao dhidi ya magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya nishati zisizofaa kama ugonjwa wa macho kwa kutumia nishati ya kuni na mkaa  

 

Kwa upande wake Bi Martha Joseph Kaloli ambae ni mnufaika wa mpango huo kutoka kata ya Nyamanoro licha ya kushukuru kwa utekelezaji wa mpango amefafanua kuwa mpango umemsaidia kujikwamua kiuchumi kwani ameweza kuanzisha miradi midogo midogo inayomsaidia katika kusomesha watoto, kulipia gharama za chakula na kuendesha maisha yake ya kila siku huku Bi Joyce Peter kutoka kata ya Ibungilo akiwaasa walengwa wenzake kutumia vizuri fedha wanazozipata kupitia mpango huo wa kunusuru kaya masikini ili mradi utakapokoma waweze kujitegemea kiuchumi 

 

Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) kwa kushirikiana na Manispaa ya Ilemela umeendelea kutekeleza mpango wa kunusuru kaya masikini katika mitaa yake yote 171 na kwamba fedha zimekuwa zikihawilishwa kwa walengwa mmoja mmoja huku miradi mbalimbali ikitekelezwa kupitia mpango huo kama barabara, shule na zahanati kwa lengo la kuwaondolea wananchi umasikini.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA ASILIMIA 10 November 21, 2025
  • ORODHA MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO WALIOTEULIWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2025 JIMBO LA ILEMELA October 20, 2025
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA VYUMBA VYA BIASHARA October 16, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • ILEMELA YAANZA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI 2026/2027

    November 25, 2025
  • "UPANDAJI WA MICHE YA MATUNDA UWE ENDELEVU";DC MKALIPA

    November 20, 2025
  • WATAHINIWA 7912 KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2025 MANISPAA YA ILEMELA

    November 17, 2025
  • DC MKALIPA AHIMIZA VIKAO NA WAZAZI JUU YA MASUALA YA LISHE MASHULENI

    November 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.