• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WAPATIWA MAFUNZO YA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO

Posted on: March 18th, 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la SOS children’s village linaendelea na utoaji wa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanaojitolea ,maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata ikiwa ni sehemu ya kuchochea malezi bora ndani ya familia kupitia mradi wa kuimarisha familia.

Akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mafunzo hayo mratibu wa dawati la watoto Idara ya maendeleo ya jamii Ilemela Bi.Sarah Nthangu amewataka wahudumu hao kuwa mfano wa kuigwa  katika kuhakikisha kuwa wanaelewa vizuri masuala ya malezi na makuzi ya watoto na wanatoa malezi bora kwa familia zao kwani wao ndio taswira halisi ya kitakachoonekana baada ya zoezi hilo.

Akifungua mafunzo hayo kaimu meneja miradi SOS children’s village Mwanza Elizabeth Swai amesema familia zinapaswa kulea watoto wao kwa malezi bora na kuimarisha upendo kwa watoto ili kuwaondolea mawazo hasi ya kutoroka majumbani na kuleta ongezeko la watoto wa mitaani .

“..Tunawajibika kuwalea watoto wetu kwa upendo ,watoto wanapaswa kulelewa na baba na mama kwa pamoja ni matamanio ya kila mzazi na familia kwa ujumla kupata mtoto mwenye maadili mazuri..”

Nae mratibu wa mradi wa kuimarisha familia kutoka shirika hilo Bi.Kokutona Kayungi amesema yapo mafanikio mengi yaliyoonekana kwa kuwahudumia walengwa ambao ni familia zinazoishi katika mazingira hatarishi toka kuanzishwa kwa mradi huo ambapo mwaka 2024 mradi ulitekelezwa ndani ya kata nne za Kayenze,Sangabuye,Bugogwa na Shibula huku akifafanua kuwepo kwa ongezeko la kata za kuzihudumia za Kirumba,Ilemela,Buswelu,Nyamhongolo na Kahama kwa bajeti ya mwaka huu 2025.

“..Mpango wa kuimarisha familia unawawezesha kuinuka kiuchumi na kuweza kuhudumia familia zao.Tunataka jamii yenyewe iwe na uwezo wa kuhudumia walengwa ,kusaidiana na kuwezeshana wao kwa wao.”

Moses Mapolu ni miongoni mwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutoka kata ya Sangabuye katika mtaa wa Igalagala yeye anapongeza shirika hilo kwa kuona umuhimu wa kuishirikisha jamii katika masuala ya malezi na makuzi ya watoto kwa kuzingatia kuwa malezi ndiyo yanayomtengeneza mtoto kuwa anavyoonekana anapokuwa mkubwa.

Mafunzo hayo maalum yenye lengo la kupata wakufunzi walioiva kila kona ya malezi na makuzi ya watoto yanafanyika kwa siku tano mfululizo kuanzia leo 17 hadi 21 Machi 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.