• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAFANYAKAZI HODARI 22 ILEMELA WATUNUKIWA VYETI NA FEDHA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 12

Posted on: May 3rd, 2023

Kiasi cha Shilingi Milioni 12 kimetolewa kwa wafanyakazi hodari 22 wa mwaka 2023 kutoka katika Idara mbalimbali za Manispaa ya Ilemela, hayo yamebainishwa na Bi Joanitha Baltazar ambae ni Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Manispaa ya Ilemela.


Fedha hizo zimetolewa kwa watumishi hao katika sherehe ya siku ya wafanyakazi Duniani zinazoadhimishwa kila mwaka siku ya  Tarehe 01 Mei ikiwa ni pongezi kwao kwa ajili ya kazi bora, utii, uadilifu na kutimiza wajibu wao katika vyeo ambavyo wanavitumikia

Katika sherehe hizo ambapo kwa mkoa wa Mwanza ziliadhimishwa katika Wilaya ya Sengerema, zikiambatana na kauli mbiu isemayo  “Mishahara Bora na Ajira za Stara ni Nguzo ya Maendeleo ya Wafanyakazi." Wakati ni sasa; Huku Mgeni Rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima ambapo aliwataka watumishi kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na uadilifu, huku akiwataka waajiri kuhakikisha wanazingatia sheria za kazi kwani kinyume na hapo hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yao.


Katika nyakati tofauti watumishi waliotunukiwa tuzo za ufanyakazi hodari katika Manispaa ya Ilemela walikuwa na haya ya kusema;


Imelda Chundu Mtendaji wa Kata ya Mecco yeye amemshukuru Mwenyezi Mungu pamoja na uongozi wa Halmashauri kwa kumuona anafaa, huku akisema kuwa anatamani sana kufanya mengi mazuri kwa kujituma na kuhakikisha shughuli za maendeleo zinafanyika kwa kiwango.


“Ninatamani sana kufanya mengi mazuri kwa kujituma zaidi katika kuhakikisha shughuli za maendeleo zinafanyika kwa kiwango kinachostahili kwa msaada wa Mungu”, amesema Imelda

Nae Musa Zuberi Afisa TEHAMA amemshukuru Mhe. Rais wa Ja,huri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji wake wa kazi ambao umekuwa chachu kwa watumishi wa chini kuchapa kazi kwa bidii zaidi ili kuendeleza nchi.


Violencea Mbakile, ambae ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini yeye amemshukuru Mwenyezi Mungu kwa tuzo hiyo ya ufanyakazi hodari, pamoja na hayo amesema kuwa yeye anaamini kujituma zaidi katika kazi ikiwa ni pamoja na kufuata sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa Umma na kubwa zaidi ni kuipenda kazi yake huku akiahidi kuendelea kuitumikia nafasi yake kwa uadilifu na ushirikiano kwa watumishi wenzake.

Mkuu wa divisheni ya utawala na Rasilimali watu, Bi Leokadia Humera amewapongeza watumishi hao na kuwataka waendelee kufanya kazi kwa bidi ili waweze kuwa chachu kwa watumishi wengine.


Zawadi ya Fedha na vyeti vilitolewa kwa; walimu wa shule za msingi za Kabangaja na Bulola, mwalimu kutoka shule ya sekondari Bwiru wavulana, afisa misitu msaidizi, afisa mipango (ii), mtendaji wa kata, afisa kilimo msaidizi, afisa uvuvi, afisa tehama, afisa manunuzi, afisa biashara, mkaguzi wa ndani (ii), msaidizi wa kumbukumbu, mwandishi mwendesha ofisi, mtendaji wa mtaa, mwandishi wa vikao (ii), mhasibu (ii), muuguzi kutoka kituo cha afya cha sangabuye, afisa maendeleo ya jamii mkuu, afisa afya mazingira msaidizi, mkuu wa divisheni ya elimu ya awali na elimu msingi na mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini.

Kati ya watumishi hao 22 waliopata ufanyakazi hodari, watumishi 20 walipatiwa kiasi cha Shilingi laki tano kila mmoja na watumishi wawili walipatiwa Shilingi Milioni moja kila mmoja.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.