• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAFANYABIASHARA WASIOSHIRIKI USAFI WA MWISHO WA MWEZI KUCHUKULIWA HATUA

Posted on: November 30th, 2024

Wafanyabiashara wasioshiriki zoezi la usafi wa kila jumamosi ya wiki la mwisho wa mwezi na waharibu wa mazingira kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kulipa faini au kufikishwa mahakamani ili kulinda mazingira yanayowazunguka na usafi wa maeneo yao

Hayo yamesemwa na afisa afya na mazingira wa manispaa ya Ilemela Bwana Peter Yohana Singu wakati wa zoezi la usafi wa kila mwisho wa mwezi lililofanyika katika soko la Kiloleli kata ya Ibungilo ambapo amesema kuwa zipo sheria zinazoelekeza jamii kufanya usafi na kulinda mazingira yanayowazunguka hivyo kitendo cha baadhi ya wafanyabiashara kujificha wakati wa shughuli za usafi na wengine kuendelea na shughuli zao hakikubali na si cha kiungwana 

‘.. Hata vitabu vya dini si vinasema mtu anapokosea unamuita mara ya kwanza unamkanya, mara ya pili unamkanya, mara ya tatu hakuna tena kumkanya kwa mdomo unachukua hatua, kwa sababu ndivyo binadamu tulivyo kama kusingekuwa na sheria kila mmoja angekuwa anafanya anavyotaka ..’ Alisema

 

Aidha Ndugu Peter mbali na kuahidi kuwapatia vifaa vya usafi watu wa eneo hilo amewapongeza wafanyabiashara wa ndizi katika soko la Kiloleli kwani wamekuwa mstari wa mbele katika kushiriki zoezi la usafi katika eneo lao pamoja na kulinda mazingira yao tofauti na wafanyabiashara wengine ndani ya soko hilo ambao wamekuwa wakifanya usafi kwa kusuasua na wengine kumuachia wakala wa eneo hilo kufanya usafi peke yake jambo ambalo si jema

 

Kwa upande wake katibu wa kamati ya usafi katika soko la Kiloleli Ndugu Hakeem Abdul amewasihi wafanyabiashara wa soko hilo kutekeleza agizo la serikali la kufanya usafi kwa kila mwisho wa wiki ya mwezi na kwamba usafi huo usiishie tu eneo la soko bali hata majumbani kwao wanapoishi huku akiongeza kuwa wao kama wafanyabiashara wa soko la Kiloleli wanatumia uchafu kama fursa kwani wamekuwa wakitengeneza mkaa kutokana na uchafu unaotokana na bidhaa ya ndizi

 

Baraka Amri ni afisa usafi na mazingira katika kata ya Ibungilo ambapo amesema kuwa suala la usafi ni la kushirikiana na kila mmoja kutimiza wajibu wake kati ya wafanyabiashara wa soko la Kiloleli na wakala wao badala ya kuachia upande mmoja wa wakala peke yake kwani wafanyabiashara wasoko hilo nao wanaowajibu wa kufanya kuhakikisha mazingira yao yanakuwa safi na salama

 

Joachim Mjuni na Prisca Innocent ni wafanyabiashara wa soko la Kiloleli ambapo wameshukuru kwa zoezi la usafi wa mwisho wa mwezi kufanyika katika soko lao kwani limewahamasisha na kuwakumbusha wajibu wao katika kufanya usafi wa mazingira yanayowazunguka huku wakiwaomba wafanyabiashara wenzao kutopuuza suala la usafi kwani ni la faida kwao binafsi kwa kujikinga na  magonjwa yakiwemo ya mlipuko kama kuharisha na kipindupindu yanayotokana na uchafu wa mazingira

 

Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.