• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO WTAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO WILAYANI ILEMELA KUJIENDELEZA KIUCHUMI

Posted on: March 29th, 2017


WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO WILAYANI ILEMELA KUJIENDELEZA KIUCHUMI

Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ya Ilemela Daktari Leonard Masale amewataka wafanyabishara ndogondogo kwa jina jingine wamachinga  wanaopatikana katika kata zilizopo wilayani Ilemela  kutumia fursa mbalimbali zilizopo wilayani humo kwa ajili ya kujiendeleza kiuchumi.

Rai hiyo ameitoa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa kwa ushirikiano wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Integrity Foundation Society na Idara ya maendeleo ya jamii ya Manispaa ya Ilemela.

Pamoja na hayo amewataka kufatilia bajeti zinazotengwa na halmashauri kwa shughuli mbalimbali za kimaendeleo sambamba na kutumia fursa zote za kujikwamua kiuchumi zinazojitokeza katika maeneo yao yakiwemo mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa wilayani humo


Akisisitiza umuhimu wa mafunzo hayo Afisa Maendeleo ya jamii wa Manispaa ya Ilemela ndugu Sitta Singibala amewataka wafanya biashara hao kuyatumia mafunzo waliyoyapata kuweza kukuza mitaji yao sambamba na kuongeza ufanisi wa bidhaa wanazozizalisha ili kuleta ushindani katika soko na kuyafikia malengo ya serikali ya nchi ya viwanda sanjari na uchumi wa kati.

Nae Mkufunzi wa mafunzo hayo ya ujasiriamali Bwana Isaac Mnyangi kutoka Integrity Foundation Society amewataka wafanyabiashara hao kuwa na mawazo tofauti kwa kutofikiria kuajiriwa huku akiwasisitiza juu ya kueshimu miiko ya biashara kwa kutofanya biashara kwa mazoea, “Watu waliosoma ujasiriamali wana uhakika wa maisha hivyo fikirieni tofauti na mkafanye biashara zenu kwa umakini na si mazoea”, alisisitiza.


Miongoni mwa wanufaika wa mafunzo hayo Ndugu Allan Kasembo kutoka kikundi cha wajasiriamali wa soko la Kirumba amesema kuwa atayatumia mafunzo aliyoyapata katika kujiongezea kipato kwa kufanya biashara tofauti na awali huku akiomba uwepo wa utaratibu wa mara kwa mara wa utoaji wa mafunzo


Nao Zena Yasini na Martha James wa kata ya Pasiansi na Kirumba wameishukuru Ilemela kwa kuanzisha utaratibu wa kutoa elimu za ujasiriamali katika kuwasaidia kujikwamua, kuzitambua pamoja na kuzitumia fursa zilizopo. “Tunashukuru kwa mafunzo haya yanayotolewa na manispaa yetu, tunaamini baada ya kuisha kwa mafunzo tutaweza kuzitambua na kuzitumia fursa zilizopo”, walisema.

Mafunzo haya ya ujasiriamali ni zoezi endelevu ambalo limelenga kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara ndogondogo katika masoko yote yanayopatikana wilayani Ilemela



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.