• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAFANYABIASHARA ILEMELA WAASWA KURUDI MAENEO RASMI YALIYOTENGWA

Posted on: October 2nd, 2023

“ Ni lazima kujali usalama na usafi wa mazingira wakati na baada ya biashara,DC peke ake,ofisi ya Mkurugenzi na wataalam wake hawataweza ndo maana tumeitana hapa ili tuwe na uelewa wa pamoja kama timu tukikaribisha ushauri na maoni yenu katika kuboresha masoko yetu.”


Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Elias Masala wakati wa kikao kazi kilichojumuisha Watendaji wa kata,watendaji wa mitaa,viongozi wa wafanyabiasha na wamachinga Ilemela,wataalam wa masuala ya masoko wa halmashauri kwa lengo la kushauriana na kuweka namna bora itakayowarudisha wafanyabiashara katika maeneo yao rasmi ya kufanyia biashara.


Akitoa taarifa juu ya hali ya utendaji wa masoko Afisa masoko wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Bi. Bertha George amesema pamoja na mafanikio mengi ambayo yamepatikana kama vile kuwepo kwa vyama vya ushirika katika masoko hali iliyowarahisishia kupata mikopo yenye riba nafuu,amazitaja changamoto ambazo ni baadhi ya wafanyabiashara kutotii sheria.

“ Changamoto kubwa kwa sasa ni wimbi kubwa la wafanyabiashara kuhamia maeneo ya barabarani na maeneo mengine ambayo sio rasmi hali inayoipa ugumu manispaa kuwafikia wote na kupata idadi halisi ya wafanyabiashara katika maboresho ya huduma mbalimbali ndani ya masoko rasmi.” Amesema Bertha


Akifafanua umuhimu wa wafanyabiashara kurudi kwenye maeneo yao Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Masala amesema ni jukumu la uongozi mzima wa wilaya kuhakikisha wafanyabiashara wote wanarudi kwenye maeneo yao rasmi yaliyotengwa kwa usalama wao.


Aidha amewataka watendaji wa kata na mitaa na wenyeviti wa mitaa kusimamia zoezi la kuwarejesha wafanyabiashara kwenye maeneo yao rasmi na kuongeza kuwa ipo miundo mbinu rafiki kwenye maeneo hayo kama vile taa kwa ajili ya nyakati za usiku ,mabanda yenye vivuli ,maji,barabara na mitaro ya maji.


“ Mtu anakaa barabarani kufanya biashara mahali ambapo ni hatarishi na viongozi wa maeneo hayo wapo hata ikitokea gari imefeli breki madhara yake ni makubwa na tutapoteza nguvu kazi ya taifa hili.Kama kuna cha kushauriana tushauriane ili tuvuke hapa lengo letu ni kuhakikisha wananchi wetu wanakuwa salama wao wenyewe na biashara zao. ”

Elimu ya mlipa kodi imetolewa na mtaalam kutoka mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Meneja cha kituo cha kodi Buzuruga Musa Haruni ambae ametoa tafsiri ya kodi kuwa ni tozo ya lazima inayotakiwa kulipwa na mfanyabiashara kwa mujibu wa sheria.


Ndugu Musa amesisitiza kuwa sheria ya kodi ya mwaka 2015 inawataka wafanyabiashara kutoa risiti wanapouza bidhaa zao.Sheria hiyo pia inamtaka mfanyabiasha mwenye mzunguko wa mauzo wa shilingi milioni 1 kwa mwaka kuwa na mashine ya kieletroniki (EFD) na mwenye mzunguko chini ya kiwango hicho kuwa na vitabu vya risiti.

“ Ieleweke kwamba wafanyabiashara wote wanapaswa kulipa kodi kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 138.Pia usipotoa risiti adhabu yake ni faini ya shilingi milioni 1.5 au asilimia 20 ya bidhaa uliyouza,kutokuwa na risiti ni kosa la jinai.”


Nae OCD wa Ilemela Afande Ignus amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa weledi kwa kuwaelewesha wafanyabiashara umuhimu wa wao kufanya biashara maeneo rasmi ili kujiepusha na matumizi ya nguvu yasiyokuwa ya lazima .


Mary Marwa ni Makamu mwenyekiti wa machinga Ilemela yeye ameshauri wazo liliowahi kujadiliwa la uwepo wa dawati la kupokea kero na maoni mbalimbali ya wafanyabiashara lifanyiwe kazi haraka ili kupunguza mkanganyiko kwa wafanyabiashara kwani wengi hawajui pa kupeleka maoni yao.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.