• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIONGOZI WANAWAKE WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA KORONA

Posted on: April 7th, 2020

Viongozi wanawake wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona unaosababishwa na virusi vya Covid-19 kwa kuelimisha familia zao na jamii inayowazunguka juu ya athari za ugonjwa huo na namna ya kujikinga.

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula wakati akizungumza na viongozi wanawake kutoka kata 19 za manispaa ya Ilemela katika ukumbi wa Monarch Hotel juu ya kuunga mkono jitihada za Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona ambapo amewataka wanawake hao kuhakikisha wanachukua hatua mbalimbali za kujikinga na ugonjwa huo sanjari na kukinga familia zao na jamii inayowazunguka kwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalamu wa afya ili kuzuia ugonjwa huo kuenea zaidi


‘.. Kwasababu nyinyi ni wana Ilemela na ni viongozi ambao tunatarajia mpate elimu na muifikishe katika jamii inayowazunguka,  Kwahiyo katika hili kongamano lengo letu ni kuwapa elimu ya tahadhari ya kujikinga na ugonjwa wa Corona ..’ Alisema


Aidha Mhe Dkt Mabula amewataka wanawake hao kuhakikisha wanazuia watoto waliopo majumbani kuzurura ovyo, kukaa katika mikusanyiko, kuchangia vyakula kwa njia ya mdomo ili kujikinga na ugonjwa huo.


Kwa upande wake mwakilishi wa mganga mkuu wa manispaa ya Ilemela, ambae pia ni mratibu wa elimu ya afya kwa jamii Bi Rose Nyemele ametaja dalili za ugonjwa wa Korona ikiwemo kikohozi kikavu, mafua makali, kuumwa na kichwa, kutapika na kupumua kwa shida,


Nae Bi Stella Mbura ambae ni afisa ustawi wa jamii manispaa ya Ilemela akitaja njia za kujikinga na ugonjwa huo ikiwemo kutokaa katika mikusanyiko ya watu wengi, kunawa mikono na sabuni kwa maji yanayotiririka, kujizuia na safari zisizo za lazima.


Moja ya viongozi waliohudhuria kongamano hilo kutoka kata ya Kahama Bi Bertha Nicholous ameishukuru taasisi ya Kivulini, manispaa ya Ilemela, Benki ya Azania na ofisi ya mbunge wa jimbo la Ilemela kwa kuendesha kongamano hilo la elimu ya Korona na ujasiriamali katika kumkomboa mwanamke kiuchumi.


Akihitimisha kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela ambae pia ndie mkuu wa idara ya ardhi na mipango miji Ndugu Shukran Kyando amewataka wanawake hao mbali na kuchukua tahadhari za ugonjwa wa Korona kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu za mipango miji sambamba na kupima maeneo yao na kuyamiliki kisheria ili kujiepusha na migogoro ya ardhi inayotokea baada ya familia kutengana au kufariki mmoja wapo.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.