• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Viongozi wa dini watakiwa kusaidia kupunguza unyanyapaa kwa WAVIU ndani ya Jamii

Posted on: February 8th, 2021

Kamati ya kudhibiti Ukimwi wilaya ya Ilemela imewataka  viongozi wa madhehebu ya dini kwaajili ya kusaidia kupunguza unyanyapaa kwa watu wanaoishi na virusi vya ugonjwa wa ukimwi (WAVIU)

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ambae pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe. Manusura Lusigaliye wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kufuatilia shughuli mbalimbali zinazotekelezwa chini ya kamati hii katika udhibiti wa ugonjwa huo ambapo amesema kuwa ipo haja ya kuwashirikisha viongozi wa dini katika kupunguza dhana potofu zinazochangia kuacha matumizi ya dawa na unyanyapaa kwa watu wanaoishi na ugonjwa huo

‘... Tutumie rasilimali zetu zote kuhakikisha tunawasaidia watu hawa, tunazo fedha tunazotenga kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma juu ya ugonjwa huu, Tuzitumie fedha hizo kwaajili ya kuwaelimisha wananchi wetu, lakini pia tusiache kuwatumia viongozi wa dini kwaajili ya kupunguza unyanyapaa ...’ Alisema

Aidha Mwenyekiti huyo ameshauri kuhamasishwa kwa vikundi vya WAVIU  vilivyopo ndani ya Manispaa ya Ilemela kuchangamkia fedha za mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu zinazotolewa kulingana na makusanyo ya mapato ya ndani sanjari na kutengwa kwa ruzuku isiyorejesheshwa kupitia kamati ya Ukimwi itakayosaidia vikundi vya WAVIU  vinavyofanya vizuri huku akitolea mfano wa kikundi cha LWIDIMA Group kilichopo kata ya Nyamanoro kinachojihusisha na shughuli za uzalishaji wa bidhaa Lishe

Nae mjumbe wa kamati hiyo ambae pia ni diwani wa viti maalum kutoka kata ya Nyamhongolo Mhe Saphia Mkama akaomba kukamilishwa kwa ujenzi wa majengo ya Zahanati ya Nyamhongolo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kiafya kwa WAVIU sambamba na kuzingatia suala la usiri pindi wateja hao wanapofuata huduma kituoni hapo

Kwa upande wake Ndugu Sitta Singibala aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela akafafanua kuwa manispaa imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya vikundi vinavyojihusisha na uzalishaji mali hivyo si vibaya kwa vikundi vya WAVIU navyo kuomba fedha hizo japo vipo vigezo na masharti ikiwemo umri kwa vijana na jinsia kwa watu wazima ingawa kamati ina uwezo wa kutenga ruzuku ambayo haina kigezo chochote na hairejeshwi kwa ajili ya kuwakwamua wananchi hao

Moja ya mwana kikundi cha Lwadina kilichopo kata ya Nyamonoro kinachosimamiwa na taasisi ya Shaloom Bi Joanitha Deus ameishukuru kamati ya kudhibiti Ukimwi ya wilaya ya Ilemela kwa kukitembelea kikundi chao sanjari na kuahidi ushirikiano na Serikali katika kutatua changamoto zinazo wakabili huku akisisitiza kuwa muathirika si sababu ya kutojihusisha na shughuli za kujiondolea umasikini

Kamati ya Ukimwi robo ya pili kwa Mwaka wa fedha 2020/20212 Manispaa ya Ilemelailifanya ziara katika taasisi ya Shaloom Care House Nyamanoro,  Kikundi cha akina mama wanaoishi na virusi vya ukimwi kiitwacho LWIDINA Nyamanoro, zahanati ya ELCT Nyakato na zahanati ya Nyamhongolo.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "TUUFANYE USAFI KUWA NI TABIA YA KUDUMUA": ANNA MBAO

    May 31, 2025
  • WATAALAM WA MANISPAA YA ILEMELA WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA MFUMO WA MANUNUZI WA UMMA

    May 29, 2025
  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.