• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Viongozi wa dini watakiwa kuiunga serikali mapambano dhidi ya UVIKO-19

Posted on: October 6th, 2021

Viongozi wa dini wametakiwa kuiunga mkono Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 kwa kuhakikisha wanaelimisha waumini wao juu ya umuhimu wa kuchanja na kuchukua tahadhari kwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalam wa afya.


Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala wakati wa kikao kazi na viongozi wa dini kilichofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Ilemela kwa lengo kukumbushana juu ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 ambapo amewataka viongozi hao kwenda kwa waumini kutoa ufafanuzi juu ya umuhimu wa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huo


“.. Serikali inao wajibu wa kuwalinda na kuwachunga wananchi wake kimwili, Lakini nyie wenzetu mnao wajibu wa kuwachunga kiroho hivyo mtagundua kazi tuliyonayo ni moja, Ni wajibu wetu kuwalinda watu hawa kwa namna yeyote ile ...’ Alisema

Aidha Mhe. Masala mbali na kuwataka viongozi hao kumshukuru Rais Mhe Samia Suluhu Hasan kwa kugharamia chanjo zinazotolewa bure kwa wananchi amewaomba viongozi hao kuhakikisha wanashiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi kikamilifu ili kusaidia utekelezaji wa mipango ya maendeleo inayopangwa na Serikali kwa kuhamasisha waumini wao kujitokeza na kuhesabiwa wakati utakapofika sanjari na kuwaomba kuzingatia sheria na taratibu za uendeshaji wa ibada kwa kutokusababisha kelele kwa wananchi wengine


Nae Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula alisistiza suala la wote kuwa na kauli moja ya kuwa na nia thabiti  ya kuhakikisha tunajikinga na korona na kuwa suluhu iliyofikiwa kwa sasa ni kupata chanjo,

Aliongeza kusema kuwa wananchi hawajazuiliwa kujifukiza na kuwa chanjo ni hiari ila akili yako ikufikishe mbali kwani Taifa haliwezi kuwa salama kama kuna wengine hawajafikia kinga iliyofikiwa

“Kama wana ilemela tuungane na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  kuhakikisha tunadumu katika maombi Mungu atuepushe na gonjwa hili, tupate chanjo, tusaidiane kutoa elimu juu ya ugonjwa huu”, Alisisitiza

Askofu Dkt Robert Bundala ambae ni mratibu wa kamati ya Amani ya mkoa akichangia katika mkutano huo amehimiza kuwa ni vyema kuelezana ukweli kuwa unapochelewa kupata chanjo unakaribisha kifo.


Nae Shekh Hasan Yasin Mchondo kutoka kata ya Kiseke mbali na kuipongeza Serikali na viongozi wake kwa hatua wanazochukua katika kupambana na ugonjwa huo wamewataka viongozi wenzao wa dini kuungana na Serikali katika kutoa elimu na kuhamasisha waumini juu ya umuhimu wa chanjo huku wakiahidi kuwa mstari wa mbele kwa hao wenyewe kujitokeza na kuchanja lakini pia kuhamasisha wengine kuchanjwa.


Katika kuhitimisha mkutano huo Mganga mkuu wa Manispaa ya Ilemela, Daktari Samson Marwa amewatoa hofu viongozi hao wa dini na kuwaeleza  kuwa Serikali kupitia wataalam wake wa ndani imefanya utafiti wa kina juu ya chanjo hiyo, hivyo kuwaomba kujitokeza kwa ajili ya kuchanja na kusisitiza kuwa kila kata imepatiwa chanjo za kutosha kwa ajili ya wananchi wa eneo husika  

“Jilinde nikulinde UVIKO-19 unazuilika, kachanje sasa”




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.