• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIKUNDI VYA WANAWAKE NA VIJANA ILEMELA VYAHIMIZWA KUTUMIA MIKOPO KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

Posted on: June 5th, 2017

VIKUNDI VYA WANAWAKE NA VIJANA ILEMELA VYAHIMIZWA KUTUMIA MIKOPO KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA


Picha ya pamoja ya wanufaika wa mkopo na viongozi wa Manispaa ya Ilemela  baada ya kupatiwa mikopo

Vikundi vya ujasiriamali vya Wanawake na vijana katika halmashauri ya Manispaa ya Ilemela vimetakiwa  kuzitumia fedha walizokopeshwa kwa ajili ya malengo yaliyokusudiwa pamoja na kurejesha kwa wakati. Hayo yalisemwa na Mstahiki Meya Mhe.Renatus Mulunga  wakati wa zoezi la utoaji wa mikopo.

“Fedha hii ambayo mmekopeshwa ikafanye shughuli za kimaendeleo na sio vinginevyo ili kuweza kurejesha kwa wakati”.Alisisitiza Mstahiki Meya

Nae Mwenyekiti wa kamati ya huduma za kiuchumi, Mhe Sarah Ngh’wani aliwasisitiza wanufaika wa mkopo huo kwa kuwataka wakazitumie fedha hizo katika kuendeleza miradi iliyopo na sio kuanzisha miradi mipya.

Aidha aliwashauri kuwa vikundi viwe na miradi ya pamoja kama vile ufugaji, kutengeneza matofali na kuongeza kwa kusema kuwa hata ile fedha Tsh.Mil.50 ya Mheshimiwa Rais itatolewa kwa vikundi vyenye miradi inayofanya vizuri.

Katika zoezi hilo la utoaji wa mikopo, vijana walihimizwa suala zima la uaminifu kwa kuwasihi kurejesha mikopo kwa wakati ili kuwezesha vijana wengine kupata mikopo, hayo yalisemwa na katibu wa vijana CCM Mkoa wa Mwanza Bi Mariam Abdallah aliyehudhuria hafla hiyo fupi.

Nae mwakilishi wa vikundi vya vijana vilivyopatiwa mikopo hiyo wakati akitoa shukurani kwa kupatiwa mikopo hiyo, aliwasilisha ombi la kuanzishwa kwa mabaraza ya vijana ili kuweza kupata sehemu ya kusemea matatizo pamoja na kutoa mawazo yao.

Jumla ya fedha kiasi cha Tsh. Milioni 70 zilitolewa kwa vikundi 35 ambapo vikundi 29 ni vya wanawake na vikundi 6 ni vya vijana kutoka katika kata 19 za Manispaa ya Ilemela ambapo zoezi hilo la utoaji wa mikopo lilitanguliwa na mafunzo ya siku moja kwa vikundi vilivyokidhi vigezo lengo ikiwa ni kuwafunza namna ya matumizi bora ya mikopo na urejeshwaji wake.






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.