• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIJANA WAHAMASISHWA KUJIHUSISHA NA KILIMO

Posted on: March 18th, 2024

Vijana wa kitanzania wamehamasishwa kujiajiri katika sekta ya kilimo kwani sekta yenye fursa nyingi za kujikwamua kiuchumi na yenye masharti nafuu katika uendeshaji wake badala ya kutegemea kuajiriwa pekee


Rai hiyo imetolewa na mkuu wa divisheni ya kilimo, mifugo na uvuvi wa manispaa ya Ilemela Bi Neema Semwaiko wakati wa ziara ya mafunzo ya wanafunzi wa mwaka wa pili idara ya jiografia na mazingira kutoka chuo kikuu cha Dodoma  ambapo amewataka vijana kuziona fursa zilizopo katika kilimo na kuitumia sekta hiyo kama mbadala wa ajira na kujiingizia kipato


‘.. Tumewapitisha vijana kwenye maeneo mbalimbali ya mijini ambapo wamejionea namna kilimo kinavyoweza kufanyika mijini na ukapata chakula na fedha, Wamekutana na vijana wenzao ambao wanalima na wanajipatia fedha, Kusoma sio lazima uajiriwe unaweza ukasoma na ukajiajiri kwenye kilimo na ukaendesha maisha yako vizuri ..’ Alisema


Aidha Bi Semwaiko ameongeza kuwa Serikali imekuwa ikiwekeza fedha nyingi katika sekta hiyo ikiwemo mafunzo na uanzishwaji wa benki ya kilimo TADB ambayo kwa kiasi kikubwa inasaidia wakulima hasa katika kujipatia mitaji hivyo kuwaomba vijana kujikita katika sekta hiyo



Daktari Enock Makupa ni mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dodoma ambapo mbali na kuishukuru manispaa ya Ilemela kwa ushirikiano kwa wanafunzi wake katika kufanya utafiti na kujifunza kwa vitendo wakati wa ziara yao ndani ya manispaa hiyo, ameongeza kuwa lengo kuu la ziara yao mbali na kujifunza pia ni kuunga mkono jitihada za serikali katika kuwaanda vijana kuanza kufikiria namna bora ya kuajiri badala ya kufikiria ajira za serikali peke yake huku akiwaasa vijana kubaini fursa zilizopo katika jamii sanjari na kuyatumia matatizo yaliyopo kuwa fursa



Donesphory  Sebarua na Prisca Dotio Francis ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma idara ya geografia na mazingira kwa nyakati tofauti wamesifu utaalam wa ulimaji wa kisasa kwa kutumia eneo dogo kwa maeneo ya mjini unaojulikana kama KICHUGUU CHA JIKONI  waliokutana nao kutoka kwa moja ya wakulima wa manispaa ya Ilemela ambapo wameongeza kuwa kupitia utaalam huo wameweza kushawishika na kuanza kufikiria kujiajiri na kujiongezea kipato pindi atakapomaliza masomo yao huku wakisisitiza vijana wenzao kufikiria na kuziona fursa zilizopo ndani ya sekta ya kilimo





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.