• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIJANA 35 WAHITIMU MAFUNZO YA USHONAJI KAYENZE

Posted on: March 14th, 2025

Vijana 35, wasichana 34 na mvulana mmoja wamehitimu mafunzo ya ushonaji na elimu ya jinsia yaliyokuwa yakitolewa na chuo cha ufundi stadi Nyakato kwa ufadhili wa shirika lisilo la serikali la SOS Children Mwanza pamoja na kukabidhiwa vyerehani ili kujiajiri na kujikwamua kiuchumi

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo katika ukumbi wa ofisi ya kata ya Kayenze kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Bi Neema Semaiko amelipongeza shirika hilo kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ndani ya manispaa yake pamoja na kuwataka vijana hao kutumia mafunzo waliyoyapata kujiendeleza kiuchumi huku akikemea uzembe kwa baadhi ya vijana wasiotaka kufanya kazi na kukimbilia kwenye michezo ya kubashiri ili kupata fedha kiurahisi

‘.. Hapa duniani hakuna anaekupa pesa ya bure zaidi ya kukufanya wewe ufikiri unapewa pesa kirahisi kwa kubeti kumbe ndo mpaka kile kidogo ulichonacho kinaondoka, Wazazi tusikae kimya hata ukiangalia hapa katika wahitimu wasichana 34, mvulana mmoja maanake wanaona kama kazi ya ushonaji ni ya kike ..’ Alisema

Aidha Bi Semaiko amewataka vijana katika jamii kuacha kuchagua kazi sanjari na kutumia kila fursa inayopatikana katika jamii kuondokana na umasikini

Kwa upande wake mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii manispaa ya Ilemela Ndugu Mohamed Atiki amelipongeza shirika la SOS Children kwa mradi huo huku akiyataka mashirika mengine kuiga mfano wake na kutekeleza miradi yenye tija ya moja kwa moja kwa jamii

Nae kaimu meneja wa miradi wa shirika la SOSO Children Bi Elizabeth Swai akasema kuwa vijana waliohitimu mafunzo hayo wametoka katika mitaa ya kata ya Kayenze na kwamba jumla ya kiasi cha shilingi milioni ishirini na sita zimetumika kugharamia mradi huo ikiwemo gharama za walimu wa mafunzo kutoka chuo cha Nyakato shilingi milioni saba, ununuzi wa vyerehani 35 kwa shilingi milioni kumi na tano na laki mbili na hamsini, vitambaa vya kujifunzia majora kwa shilingi milioni tatu na laki tano

John Lucas, Senora Phabian na Jalaki Yahya ni miongoni mwa wahitimu wa mafunzo hayo ambapo wamelishukuru shirika kwa kuwapa ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuacha kuwa wategemezi huku wakiahidi kutunza vyerehani walivyokabidhiwa

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.