• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

UMMY WAYAYU: " KASIMAMIENI UKUSANYAJI WA MAPATO"

Posted on: January 15th, 2025

Watendaji wa kata na mitaa wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela, wametakiwa kuhakikisha wanasimamia suala zima la ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao ya utawalaili kuhakikisha halmashauri inafikia lengo lake.

 

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Bi Ummy Wayayu alipokutana na watendaji hao katika kikao kazi kilichohusu suala zima la ukusanyaji wa mapato siku ya tarehe 15 Januari 2025.

 

Aliendelea kuwasisitiza kuwa jukumu moja wapo la utendaji wao linahusu ukusanyaji wa mapato, bila kukusanya mapato maana yake hakuna kazi, shughuli zote za maendeleo hazitawezekana na hata ustawi wa watumishi hautawezekana, na kuwakumbusha kuwa wao ni watu muhimu sana katika eneo hili la ukusanyaji wa mapato

 

“Kasimamieni ukusanyaji wa mapato katika maeneo yenu ya utawala na kila mmoja wenu atimize wajibu wake kwa ueledi na uadilifu wa hali ya juu na kwa mtendaji ambae ataenda kinyume na maelekezo sitasita kuwachukulia hatua na kwa mwenye changamoto yoyote ahakikishe anaiwasilisha kwangu”,amesema Bi Ummy

 

Aidha amewakumbusha watendaji kuwa ni wajibu wao kuwatembelea wafanyabiashara kwa ajili ya kufuatlia kama wamekidhi mahitaji pamoja na kutoa msaada kwa wafanyabiashara ambao hawana uelewa wa namna ya kulipa tozo mbalimbali, lakini si hilo tu kuwapa uelewa juu ya namna ambavyo kodi hizo zinasaidia katika maendeleo ya nchi.

 

Herbert Bilia ni mchumi wa manispaa yeye amewataka watendaji hao kuhakikisha wanazingatia matumizi ya sheria ndogo za halmashauri katika suala zima la ukusanyaji wa mapato, huku Ndugu Kefadan Gembe ambae ni Afisa Biashara wa manispaa yeye amesisitiza juu ya suala la kuhakikisha kila mtendaji anakuwa na kanzidata sahihi  yenye vyanzo mbalimbali katika maeneo yao ili kurahisisha zoezi hilo.

 

Nae Bi. Mariam Mshana, mweka hazina wa manispaa ya Ilemela, amewataka watendaji kutumia kauli nzuri pamoja na kutoa huduma bora pindi watakapokuwa wanaendesha zoezi hilo kwani ukusanyaji wa mapato unahitaji hekima kubwa

 

Nao watendaji hao katika nyakati tofauti wameshukuru kwa kikao kazi hicho na kupokea maelekezo yaliyotolewa ambapo wameomba kupatiwa mafunzo mbalimbali juu ya masuala ya ukusanyaji wa mapato, sambamba na kuomba uwepo wa kikao kazi kama hiki kila mwezi

 

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela katika mwaka wa fedha 2024/2025 imepanga kukusanya cha shilingi bilioni 14.95 kutoka vyanzo vya ndani vya mapato fedha hizi hutumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo sambamba na uendeshaji wa shughuli mbalimbali za taasisi.

 

 

 

 

 

Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.