• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMBI YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA YAANZA KUTOA HUDUMA ILEMELA

Posted on: October 20th, 2025

Mapema leo tarehe 20 Oktoba 2025, timu ya madaktari bingwa na bingwa bobezi wa Rais Samia wamewasili Manispaa ya Ilemela kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa wananchi wa Ilemela ikiwa ni awamu ya nne toka kuanza kwa huduma hizi.

 

Dkt Delfina Mkenda (Daktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake na ukunga) ambae ni kiongozi wa timu hiyo madaktari amesema kuwa wamejipanga  kutoa huduma bora kwa wananchi wa Ilemela ili kuweza kutimiza lengo la Dkt Samia la kusogeza huduma karibu na wananchi.

 

Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Bi Ummy Wayayu, amemshukuru Rais Samia kwa kuweka utaratibu huu wa kusogeza karibu huduma za kibingwa na bobezi katika maeneo mbalimbali ya nchi hususan Ilemela kwani wananchi wanahitaji sana huduma hizi za kibingwa na bobezi ambapo ameahidi kutoa ushirikiano kwa madaktari hao

 

"Wananchi wana uhitaji wa huduma hizi ukizingatia hali ya upatikanaji wake na hali zao za kiuchumi inakuwa ni  changamoto lakini timu kama hii inapokuja inakuwa ni nafuu kwao wanapata huduma hizi kwa karibu, hivyo nimshukuru Mhe Rais Dkt Samia kwa kuweka utaratibu huu wa kuwafikia wananchi wake", amesema Mkurugenzi Ummy.

 

Sambamba na hilo, Mkurugenzi Ummy amemuelekeza mganga mkuu wa manispaa ya Ilemela, Dkt Maria Kapinga kuweka utaratibu mzuri wa kuwafikisha wagonjwa wenye uhitaji wa huduma katika hospitali ya wilaya ya Ilemela kutokana na umbali wa hospitali hiyo ili kuhakikisha lengo lililokusudiwa la kuwapatia huduma hizo wananchi linafanikiwa.

 

Kambi hii ya madaktari itatoa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi katika hospitali ya Wilaya ya Ilemela iliyopo Isanzu kwa muda wa siku tano kuanzia tarehe 20 hadi 24 mwezi huu wa oktoba, ambapo huduma zitakazotolewa ni pamoja na huduma za magonjwa ya wanawake na ukunga, watoto na watoto wachanga, upasuaji, magonjwa ya ndani na huduma za kinywa na meno.

Announcements

  • ORODHA MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO WALIOTEULIWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2025 JIMBO LA ILEMELA October 20, 2025
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA VYUMBA VYA BIASHARA October 16, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -JIMBO LA ILEMELA October 14, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA YAANZA KUTOA HUDUMA ILEMELA

    October 20, 2025
  • TIMU YA MENEJIMENTI ILEMELA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    October 16, 2025
  • DKT BITEKO AZINDUA MRADI WA PANDEMIC FUND, AELEKEZA USIMAMIZI MZURI

    October 15, 2025
  • ELIMU YA MABADILIKO YA TABIA NCHI YATOLEWA KWA MAAFISA UGANI KILIMO MANISPAA YA ILEMELA

    September 29, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.