• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

UMAKINI NA UADILIFU WASISITIZWA KWA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA MAUDHUI NA TEHAMA ILEMELA

Posted on: August 15th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hasan Masala amewataka makarani pamoja na wasimamizi wa maudhui na TEHAMA katika Wilaya ya Ilemela kuhakikisha wanakuwa makini na  waadilifu katika zoezi la sensa ya watu na makazi linatorajiwa kufanyika mnamo tarehe 23 mwezi wa nane ,2022.


Mhe Masala, ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo kwa washiriki 1346 ambayo yaliyotolewa kwa  takribani siku 19 huku akiwakumbusha juu ya kuzingatia wajibu wa kazi iliyowapeleka ikiwa ni pamoja na kuepuka upikaji wa taarifa.

“Tunaamini katika mafunzo mliyopatiwa mmeelezwa uadilifu na umakini na kazi zetu nenda kachukue dodoso ya kile kilichokupeleka ukimaliza ondoka usiende kufanya yaliyo nje na hayo na  msije kusahau wajibu wa kazi iliyowapeleka”, amesema Mhe Masala.

Pamoja na hayo amewataka washiriki wa mafunzo hayo kutambua thamani ya kazi wanayoenda kufanya kwani dhamana waliyopewa ni kubwa na kusisitizwa kutokutanguliza mbele maslahi bali kuangalia ni nini wamelifanyia Taifa la Tanzania kwani chochote watakacholipwa hakina thamani kwa kazi kubwa iliyopo mbele yao


 “Zoezi hili serikali imewekeza muda, rasilimali fedha , vifaa vyenye thamani kubwa kwa kufanya hayo yote hata wewe uliyepewa  dhamana ya kufanya kazi hii lazima utambue thamani ya kazi ambayo unayoenda kufanya usiangalie unalipwa nini angalia umeisaidia taifa lako kwa kiasi gani kufanikisha zoezi hili hiyo ndio sifa kubwa utakayoondoka


Nae mratibu wa Sensa ya watu na makazi 2022 Wilaya ya Ilemela , Ndugu Yohanne Magesa ametoa rai kwa washiriki wa mafunzo hayo kufanya kazi kwa vitendo, hiari na kwa moyo na kuwahimiza kuangalia uzalendo wa Taifa la Tanzania.

Ndugu Said Kitinga ambae ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela amewapongeza washiriki hao kwa kupata nafasi ya kuweza kushiriki zoezi la kitaifa la sensa na kuwataka kujiona kuwa wao ni wa thamani kwani wamepata nafasi ya kipekee ambapo aliwasisitiza kufanya kazi hii kwa ueledi na pia kwenda kuitumia elimu waliyopewa mara baada ya zoezi la sensa kukamilika.

Nao washiriki wa mafunzo hayo ya sensa ya watu na makazi wamemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa nasaha zake na kuzitaja changamoto zilizojitokeza wakati wakifanya mazoezi kwa vitendo likiwemo suala la baadhi ya wananchi kuonyesha kutokuwa tayari kushiriki zoezi hilo hivyo kuomba elimu zaidi kutolewa katika siku zilizobakia.

Zoezi hili la kufunga mafunzo ya Sensa ya Watu na Makazi limeambatana na zoezi la uapishwaji ambapo washiriki wote waliapishwa kiapo cha utii, uadilifu na uaminifu mbele ya Waheshimiwa mahakimu Leonard. H. Ndolezi na Cindy Kaaya na kukumbushwa kuwa kiapo kimetolewa kwa mujibu wa sheria ya Takwimu ya Sura Na 351, sheria inayosimamia masuala ya Sensa nchini huku wakionywa kutunza siri zote.










Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.