• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

"TWENDENI TUKAKUSANYE MAPATO KWA KIWANGO KIKUBWA", MEYA MULUNGA

Posted on: February 9th, 2023

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe. Renatus Mulunga amewataka waheshimiwa madiwani na watalaam kukusanya mapato kwa kiwango kikubwa ili kuweza kuitekeleza bajeti ijayo ya mwaka wa fedha 2023/2024.


Ametoa rai hiyo wakati wa kikao cha baraza la madiwani ambalo liliketi kwa ajili ya kupitia mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo amesema kuwa, suala la kupitisha bajeti ni suala moja lakini bajeti haiwezi kutekelezeka kama tulivyoipitisha kama wote kwa pamoja hatutashirikiana katika suala zima la ukusanyaji wa mapato

“Nitoe rai kwa wakazi wote wa manispaa ya Ilemela kupitia kata zetu kuhakikisha wanalipa tozo zote kama inavyowapasa pamoja na hilo niwatake waheshimiwa madiwani tuwe pamoja katika suala la ukusanyaji wa mapato kwan tukikusanya vyakutosha haya tuliyoyapitisha yataweza kutekelezeka na kama hatutakusanya tutaendelea kupitisha na utekelezaji hautafanyika” amesema Mhe Mulunga


Wakichangia bajeti hiyo kwa nyakati tofauti madiwani wamepongeza kwa namna ambavyo bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuwa imeangalia sekta mbalimbali ikiwemo suala la ukamilishaji wa miradi viporo huku wakihimiza suala la utekelezaji wa bajeti ili wote kwa pamoja tuwe mfano na kusisitiza kuwa wataalam wasimamie kwa makini ili bajeti ilete tija


Akichangia kuhusu mikopo ya asilimia 10, diwani wa viti maalum Mhe Sarah Lisso amepongeza kwa halmashauri kuwakopesha vijana na kuweza kuanzisha mradi mkubwa wa ufugaji samaki kwa njia ya vizimba huku akishauri  jambo kama hilo lifanyike pia kwa vikundi vya wanawake badala ya kupewa fedha wasimamiwe kuanzisha mradi ili waweze kujikwamua  kiuchumi.

Mhe Maganiko kutoka kata ya Nyamanoro akichangia bajeti hiyo  ameomba bajeti hiyo iangalie suala la utunzaji wa maeneo ya makaburi kwa ajili ya kuwasitiri ndugu waliotangulia pamoja na kushauri  juu ya suala la ununuzi wa greda kwa ajili ya kuboresha barabara katika kata mbalimbali za Halmashauri kwani malalamiko ni wengi kwa wananchi yanayohusiana na ubovu wa barabara.

Mhandisi Modest Apolinary, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, amefafanua masuala mbalimbali kuhusiana na bajeti na kusema kuwa hii ni rasimu ya bajeti hivyo amepokea maoni yote na kuahidi kuyafanyia kazi kabla ya kuwasilishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kusomwa katika bunge la bajeti.

Awali akiwasilisha bajeti hiyo Mchumi wa Manispaa Ndugu Herbert Bilia amesema Halmashauri imekadiria kukusanya na kutumia  jumla ya Shilingi Bilioni 71.57  ambapo kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni 8.39 ni kwa ajili ya Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo, Shilingi bilioni 45.29 ni Mishahara, Shilingi bilioni 1.65, Ruzuku ya Matumizi ya Kawaida.


Kwa upande wa mapato ya ndani Ndugu Bilia amesema kuwa Halmashauri inakisia kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 16. 23 ambapo Shilingi bilioni 8.76 kati ya fedha hizo za mapato ya ndani ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na shilingi bilioni  Tshs 5.84 ni matumizi ya kawaida na  Shilingi Bilioni 1.61 ni mapato fungwa.

Bajeti hii ya mwaka wa fedha 2023/2024 imepanda kutoka Shilingi Bilioni 67.77 ya mwaka 2022/2023 hadi kufikia Shilingi bilioni 71.57 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 5.6. Amesema ndugu Bilia.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.