• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

TFS YAENDELEA KUSHIRIKIANA NA ILEMELA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Posted on: November 24th, 2022

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela ndugu Marco Busungu amesema Ilemela inaendelea kuunga mkono jitihada za Mhe.Rais katika kutunza mazingira kwa kupanda miti mingi zaidi katika kipindi hiki ambacho mvua zimeanza kunyesha mkoani Mwanza ambapo Ilemela ni moja ya wilaya ndani mkoa huu.


Akizungumza wakati akipokea miti 5,000 kutoka wakala wa misitu (TFS)-Mwanza, Busungu amesema ni jukumu la jamii nzima kutunza miti kwa kuzingatia faida zake nyingi katika maisha ya binadamu.

"Ilemela tunaendelea  kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais Mhe.Mipango anayoendelea kuyatoa maeneo mbalimbali katika ziara zake juu ya utunzaji wa mazingira sambamba na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita katika masuala mazima ya kupambana na mabadiliko ya tabia nchi." Amesema Busungu


Alex Julias ni mhifadhi misitu na nyuki kutoka TFS -MWANZA anasema kampeni ya upandaji miti imeanzia shule za msingi kwa sababu ni sehemu inayomjenga mtoto kuwa na mazoea ya kufanya jambo mara kwa mara bila kusahau hivyo watoto wakielekezwa vizuri ni mabalozi wa kudumu katika suala la utunzaji wa mazingira.


Afisa elimu mazingira ndugu Beatus Kahulu amewashukuru TFS -MWANZA kwa wepesi wao wa kuitika wito na kujibu ombi la Ilemela kwa kutoa miche hiyo huku akiwataka walimu, wanafunzi na wazazi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha miti hiyo inatunzwa ili ilete tija ilokusudiwa.


Nae Anthony Goodlucky mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Kiseke amezitaja baadhi ya faida za upandaji miti ikiwa pamoja na miti kuzalisha hewa safi ya oksijeni,baadhi ya miti ni chanzo cha mapato mfano miti ya mbao,miti ya matunda ni faida katika masuala ya lishe bora na pia miti hutoa vivuli hasa nyakati za jua.

Jumla ya miche ya miti 5,000 iliyopokelewa kutoka TFS  imejumuisha miti ya mbao,kuni,nguzo na matunda kama parachichi .


MWISHO

Imetolewa na;

Kitengo cha mawasiliano serikalini -Manispaa ya Ilemela


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.