• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

TASAF KUWAONGEZEA UJUZI NA AJIRA WALENGWA KUPITIA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Posted on: September 2nd, 2024

Mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF umelenga kuanzisha miradi ya maendeleo itakayosimamiwa na kutekelezwa na kaya za walengwa walioandikishwa katika mpango huo kwa ngazi za mitaa kwa lengo la kuwaongezea ujuzi, ajira na kuboresha miundombinu yao


Hayo yamesemwa na mratibu wa mpango huo katika manispaa ya Ilemela Ndugu Leonard Robert Nyamgenda wakati wa zoezi la uhawilishaji fedha kwa dirisha la malipo la mwezi Mei-Juni 2024 ambapo amesema kuwa walengwa watajengewa uwezo kwaajili ya kuanzisha miradi katika maeneo yao watakayokuwa na uwezo wa kuitekeleza kwa nguvu zao wenyewe na si kwa kutumia mashine au wakandarasi


“Walengwa watafanya kazi katika miradi midogomidogo kama ujenzi wa barabara, visima na mingine watakayoona wao inafaa katika mtaa wao kwa kutumia nguvu kazi zao wenyewe kwa siku kumi kwa mwezi, kwa masaa yasiyozidi matatu na kwa ujira wa shilingi elfu tatu”, Alisema


Deograsia Lubugo ni mwezeshaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini kata ya Nyakato ambapo amesema kuwa licha ya miradi hiyo kutekelezwa na wanufaika wa mpango wa TASAF lakini pia miradi ikishakamilika itabaki kuwa mali ya jamii nzima na kwamba zipo faida nyingi zitakazopatikana kupitia uanzishwaji wa miradi ikiwemo kukuwa kwa miundombinu, ajira na kujipatia kipato.


Nae mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kangaye ‘B’ Joseph Nyabinyiri  akaongeza kuwa utaratibu wa uanzishaji wa miradi kwa walengwa utawasaidia walengwa kujiongezea

kipato cha ziada tofauti na kile kinachopatikana moja kwa moja kupitia mpango sanjari na kuwafanya kuwa na nidhamu zaidi ya fedha kwani sasa watakuwa wakipata kipato kwa kufanya kazi badala ya ile inayotolewa bila kufanya kazi yeyote pamoja na kuleta maendeleo ya pamoja katika mtaa kupitia miradi itakayotekelezwa.


Bi Rahel Shimba na Bi Nyakaho Mgaya Malemba ni wanufaika wa mpango kutoka mitaa ya majengo mapya kata ya Nyakato ambapo wameipongeza na kuishukuru serikali kuja na mpango huo kwani utasaidia kutatua kero ya ubovu wa barabara katika mtaa wao na kwamba utasaidia kutatua kero zilizo katika jamii katika maeneo mengine kulingana na uhitaji bila kutumia gharama kubwa na muda mrefu kwa kuwa kazi hizo zitakuwa zikifanywa na wanufaika wa mtaa husika.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.