• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SHULE YA SEKONDARI YA BUGOGWA YANUFAIKA NA MGAO WA KOMPYUTA

Posted on: July 11th, 2017

SHULE YA SEKONDARI YA BUGOGWA YANUFAIKA NA MGAO WA KOMPYUTA

Shirika la wamisionari la Christian Life World Mission Frontiers kupitia taasisi ya angeline foundation imeipatia shule ya sekondari Bugogwa jumla ya Kompyuta 20 ikiwa ni jitihada za Mhe Mbunge wa jimbo la Ilemela katika kuhakikisha kuwa kila shule katika Manispaa ya Ilemela inakuwa na kompyuta ili kuwawezesha wanafunzi kupata maarifa mbalimbali pamoja na kujiandaa na Tanzania ya Viwanda.


Rais wa shirika hilo la wamisionari, Mchungaji Dr Paul Kim  kutokea Korea Kusini amemuhakikishia Mbunge wa Ilemela kuwa ataendelea kuziunga mkono jitihada zake katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Ilemela huku  akiahidi kuwa ataleta wataalam ili waweze kufundisha somo la kompyuta ili kuweza kuta wataalam zaidi kwani nia yake ni kuiona Afrika na Tanzania iliyo bora.



Aliyekuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo Mbunge wa Ilemela Mheshimiwa Angeline L.Mabula alisema kuwa, lengo kubwa la kuwapatia kompyuta hizo ni kuwaandaa vijana kwenda na wakati pamoja na kujiandaa na  kuijenga Tanzania ya viwanda.


Pamoja na hayo alisema kuwa,  ni matarajio yake kuwa walimu watazitumia kwa kupata habari za kielimu pamoja na kuwafundisha wanafunzi na si kwa matumizi mengineyo.Aidha aliwasihi kuimarisha ulinzi katika shule hiyyo ili kuhakikisha kuwa kompyuta hizo haziibiwi ili kuweza kuwapa imani wafadhili na pia wajiandae kuwapokea walimu watakaoletwa kwa ajili ya kutoa elimu ya kompyuta kama wafadhili hao walivyoahidi.


“Tunapoelekea ni  Tanzania ya viwanda hivyo ni muhimu kuwa na ujuzi wa matumizi ya kompyuta hivyo  maandalizi yanatakiwa yaanze mapema.Pia nasisitiza vijana muwe makini na kufuatilia yale yanayoelekezwa na viongozi wao pamoja na kuunga juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”,Alisisitiza

Aidha hakuacha kugusia kuhusu suala la mimba huku akiwaasa wanafunzi wa kike kujitunza na kuzingatia elimu kwani ndio suala lililowapeleka hapo shuleni huku akisisitiza kuiunga kauli ya Mheshimiwa Rais kwa asilimia 100 ya kupiga mimba mashuleni.


“Huwezi kusoma ukiwa katika hali hiyo, nawasihi kuanzisha klabu za wasichana kwa ajili ya kuweza kuelimishana na pia walimu muwaone wanafunzi hao kama watoto wenu  wa ”, Alisisitiza.


Nae Mheshimiwa Diwani wa kata ya Buswelu ambae ndie Mwenyekiti wa kamati za Huduma za Uchumi, Elimu na Afya pamoja na kuwashukuru wafadhili hao na Mheshimiwa Mbunge kwa kuwapatia kompyuta hizo amewataka wanafunzi wa shule hiyo kuzitunza kompyuta hizo na kusoma kwa bidii ili ziweze kunufaisha na wanafunzi wengine.


Deus Stephano ambae ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiyo, alimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada zake na kwa wafadhili kwa kukubali kuwapatia kompyuta hizo. Alisema kuwa kompyuta hizo zitawasaidia kuendana na kasi ya dunia ya sayansi na teknolojia, huku akiahidi kuwa watazitunza ili na wanafunzi wengine watakaosoma katika shule hiyo waweze kuja kuzitumia.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "TUUFANYE USAFI KUWA NI TABIA YA KUDUMUA": ANNA MBAO

    May 31, 2025
  • WATAALAM WA MANISPAA YA ILEMELA WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA MFUMO WA MANUNUZI WA UMMA

    May 29, 2025
  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.