• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SHILINGI MILIONI 206 KUJENGA ZAHANATI KISIWA CHA BEZI

Posted on: July 16th, 2024

Serikali imetenga jumla ya kiasi cha shilingi milioni 206 kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF-OPEC 4) kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na nyumba za watumishi katika kisiwa cha Bezi wilayani ilemela ili kutatua kero ya muda mrefu ya ukosefu wa huduma za afya inayowakabili wananchi wa kisiwa hicho


Hayo yamesemwa na mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula wakati wa ziara yake katika kata ya Kayenze mtaa wa Iponyabugali yenye lengo la kusikiliza kero za wananchi na kutoa mrejesho wa vikao vya bunge kwa wananchi ambapo amesema kuwa changamoto ya wazazi kujifungulia njiani wakati wa kufuata huduma za afya umbali mrefu na Gharama kuwa kubwa imepata utatuzi baada ya serikali kuweka mpango wa kuboresha huduma za afya katika eneo Hilo


“Serikali ya awamu ya sita chini Dkt Samia Suluhu Hassan imetenga fedha kwa ajili ya nyumba za watumishi mbili kwa moja milioni 103 na zahanati milioni 103, Kikubwa tuendelee kuunga mkono jitihada za serikali”, Alisema


Aidha Mhe Dkt Mabula akawataka wananchi wa kata hiyo kusimamia na kulinda vifaa vya ujenzi wa miundombinu hiyo visiibiwe ili kukamilisha miradi mbalimbali inayotekelezwa ndani ya kata hiyo pamoja na kuwaripoti wabadhirifu wote wa mali za umma watakaojitokeza ili Sheria ichukue mkondo wake


Gabriel Remmy ni msanifu majenzi halmashauri ya manispaa ya Ilemela amefafanua kuwa mradi huo wa zahanati utakuwa na huduma za baba,mama na mtoto , huduma za wagonjwa wa nje pamoja na nyumba moja itakayojumuisha familia mbili huku akiongeza kuwa kinachosubiriwa ni mifumo ya malipo kuanza kufanya kazi ili mradi uweze kutekelezwa


Kwa upande wake diwani wa kata ya Kayenze Mhe Issa Mwalukila Dida mbali na kuishukuru Serikali na mbunge wa jimbo hilo kwa kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo akawataka wananchi wa kata yake kuchangia na kushiriki shughuli za maendeleo ili jamii yao iweze kusonga mbele.


Joachim Sylvester ni mwananchi wa mtaa wa Iponyabugali kata ya Kayenze ambapo amempongeza mbunge Dkt Angeline Mabula kwa kufanya ziara katika mtaa wao kusikiliza kero na kuzipatia ufumbuzi akiambatana na wataalam wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela pamoja na wakuu wa taasisi zinazofanya kazi zake ndani ya Jimbo la Ilemela ikiwemo TANESCO, TARULA, MWAUWASA na nyIngine


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.