• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC MWANZA AIELEKEZA ILEMELA KUFUTA HOJA ZILITOTOLEWA NA CAG

Posted on: June 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela kwa kushirikiana na timu yake ya watalaam kuhakikisha kuwa  hoja zilizotolewa na  mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG)  zinafutwa kabla ya kuelekea katika vikao vya LAAC.

Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa maelekezo hayo wakati akiendesha kikao maalum cha baraza la madiwani lililoketi kwa ajili ya kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za seikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na utekelezaji wake ambapo  Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imepata hati safi.

“Mkurugenzi shirikiana na timu yako kuhakikisha kuwa hoja hizi zilizobaki zinamalizika kabla ya kuelekea katika vikao vya LAAC kwani hizi ni hoja dhaifu ambazo zinaweza kumalizika”. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Pamoja na hayo amewataka viongozi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanaangalia  viashiria vyote hatarishi katika matumizi ya fedha, fedha mbichi isiliwe, miradi yote isimamiwe na kamati za ujenzi  huku akiwataka kuhakikisha kuwa mapungufu yaliyojitokeza hayajirudii  kwani nia na ndoto ya Mhe Rais Samia Suluhu, ni fedha zitumike na kuleta matokeo chanya katika jamii tunayoisimamia.


“Mafanikio hayaji hivihivi, ni kujituma kwa viongozi niwapongeze wote, Mbunge wa Jimbo,  Mstahiki Meya na Baraza lako, timu ya wataalaam kwa kufanikisha haya kutembea pamoja, kutambua changamoto na kuweza kuzitatua na pale inapobidi kujisahihisha, aidha nikupongeze pia  Mkurugenzi ambae ni kiongozi wa watumishi kwa kuwa msikivu na kuona kuwa maendeleo yanapatikana Ilemela, Alisisitiza Mhandisi Gabriel

Nae Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Salum Kali amesema kuwa anayo  imani kuwa maelekezo yaliyotolewa yatafanyiwa kazi na kuwa mwaka wa fedha ujao umakini utaongezeka kabla ya kutoa maamuzi

Mhe Renatus Mulunga, Mstahiki Meya wa Ilemela, amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa ushirikiano na muongozo wa kila siku ambayo imeifikisha Ilemela hapa ilipo huku akimuahidi kutekeleza maelekezo yote aliyoyatoa katika baraza.

Nikushukuru na kukuahidi ushirikiano wa kutosha na kutekeleza maelekezo yote uliyotupatia siku ya leo , kwani dhamira ni kuleta  maendeleo kwa Manispaa ya ilemela, Mhe. Mulunga

Akiwasilisha  Taarifa ya mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/2021 , Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary, amesema kuwa pamoja na Halmashauri kupata hati safi kwa mwaka uliopita wa 2020/2021 Ilemela imeendelea kupata hati safi kwa kipindi cha miaka sita mfululizo  ambapo hadi sasa hoja zilizobaki ni 11 tu.


Announcements

  • TANGAZO LA MIKOPO VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA, WATU WALEMAVU June 28, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA MTENDAJI WA MTAA November 26, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 06, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI STENDI MPYA YA MABASI NA MAEGESHO YA MALORI March 15, 2022
  • View All

Latest News

  • RC MWANZA AIELEKEZA ILEMELA KUFUTA HOJA ZILITOTOLEWA NA CAG

    June 20, 2022
  • Shule binafsi zatakiwa kujenga uhusiano na jamii

    June 14, 2022
  • Maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani- Miti 100 yapandwa katika shule ya Sekondari Buswelu

    June 03, 2022
  • Shilingi Milioni 154 zakusanywa kukabiliana na changamoto ya madawati katika shule za msingi za Ilemela

    June 01, 2022
  • View All

Video

Sensa Ya watu na Makazi tarehe 23/08/2022
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.