• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC MTANDA AMEWATAKA WAFANYABIASHARA KUFUATA SHERIA ZA NCHI

Posted on: June 5th, 2024

“Hakuna mahusiano ya uchaguzi na wafanyabiashara kufanya biashara barabarani, watu wafuate sheria kwani nchi ikienda bila sheria inakuwa ina fujo na nchi yenye fujo haiwezi kuwa nchi endelevu”.


Ni kauli iliyotolewa na Mhe Said Mtanda Mkuu wa Mkoa wa Mwanza tarehe 05 Juni, 2024 alipofika katika soko la Kiloleli katika kata ya Ibungilo kwa lengo la kukagua na kuongea na wafanyabiashara wa soko hilo ambapo amebaini  wafanyabiashara wadogo kususia Soko hilo lenye miundombinu rafiki na kujikita kwenye magulio ya mnada yanayofanyika kwenye hifadhi za barabara.


Mhe. Mtanda, amewataka wafanyabiashara wilayani Ilemela kufuata sheria za nchi kwa kufanya shughuli zao kwenye masoko rasmi na kuutaka uongozi wa Wilaya ya Ilemela kusimamia suala hilo kwa kupunguza minada ya barabarani na kuhamasisha wafanyabiashara kubaki kwenye masoko rasmi.


“Mkuu wa Wilaya ninaamini kwamba mtakaa na idara ya biashara kuhakikisha kwamba mnajipanga vizuri kupunguza hiyo minada ili maeneo rasmi yaendelee kuwa na wafanyabiashara”,Amesisitiza Mhe Mtanda


Aidha ametumia mkutano huo kuwakumbusha wafanyabiashara kuwa kufanya biashara katika maeneo rasmi ni fursa kwao, kwani benki ikikukuta eneo rasmi ni rahisi kukukopesha kuliko unapokuwa unafanya biashara kwa kuhamahama hivyo utakuwa hukopesheki.


Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa ametoa mwezi mmoja kwa uongozi wa Ilemela kuhakikisha unatekeleza maelekezo ya kuboresha miundombinu katika soko la kiloleli ili kuweza kuwavutia wafanyabiashara kuuzia bidhaa zao katika soko hilo.


Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala amesema kuwa wapo tayari kutekeleza maagizo hayo na kwamba wamejipanga kuboresha miundombinu kwenye masoko yao na kwa mwaka wa fedha unaoendelea wametumia zaidi ya Milioni 180 kukarabati miundombinu kwenye masoko lakini bado machinga wamejikita kufanya biashara kwenye hifadhi za barabara kwa kigezo cha mnada.


Kalala Magafu, ni mwenyekiti wa Soko la Kiloleli na mwenyekiti  wa wenyeviti wa masoko wilayani Ilemela kwa niaba ya wafanyabiashara wasoko hilo ameomba kufanyike maboresho kama vile kuwekewa umeme, kuongezewa vyoo pamoja na kuwekewa paa eneo la kuuzia ndizi ili kuweza kuwavutia wafanyabiashara wengine kufanyia biashara katika soko hilo, huku akitoa wito kwa wafanyabiashara wenzake kurudi kwenye soko hilo ili maeneo ya nafaka, ndizi, matunda na nguo yapate wafanyabiashara.


Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.