• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC MAKALLA: NINATOA SIKU 14 KUKAMILISHA MAJIBU YA WANANCHI

Posted on: October 18th, 2023

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, kupitia idara ya ardhi imetakiwa kuhakikisha inakamilisha majibu ya wananchi ambao wamesikilizwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza siku ya tarehe 17 oktoba 2023 akiwa katika ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Ilemela.


Maelekezo hayo yametolewa na Mhe. CPA Amos Makalla, mara baada ya kuhitimisha zoezi la kuwasikiliza wananchi waliofika kuwasilisha kero zao ambapo jumla ya wananchi 50 walisikilizwa


“Kila mwananchi aliyesikilizwa awe amejibiwa ndani ya siku 14, nataka kupima yale ambayo mkuu wa wilaya akiwaelekeza hamtekelezi, itakuwa jambo la ajabu sana iwapo malalamiko haya hayakufanyiwa kazi, niwaombe tekelezeni maelekezo haya yote tuliyoyatoa na majibu yapatikane ili tukija siku nyingine tuanze kusikiliza mambo mapya, nataka nikja Ilemela wananchi waseme yale uliyoagiza yamefanyiwa kazi”, alisistiza CPA Makalla.


Sambamba na maelekezo hayo amewataka watendaji wa idara ya ardhi kubadilika na kutoa huduma inayostahili kwa wananachi kwa kuwa lugha za kutoa huduma na matumaini kwa wananchi katika kutatua matatizo yao ya ardhi.


 “Lugha za kuwahudumia wananchi ziwe lugha za staha na zenye matumaini sitaki kuja kusikia malalamiko ya namna mnavyowapokea wananchi wetu”,


Aidha amesema kuwa amebaini kuwa mambo yaliyochangia katika migogoro ya ardhi kwa kiasi kikubwa ni pamoja na upimaji shirikishi kwani inaonesha makampuni yanayopima hayana mawasiliano na ofisi, hayaratibiwi vizuri, lakini viongozi waliopo hawasimamii na kuwajibika ipasavyo katika suala hili la upimaji shirikishi.Hivyo ametoa maelekezo kwa Halmashauri kuhakikisha inalibeba jukumu hilo.


“Suala Kupima, Kupanga na Kumilikisha (KKK), ni jukumu la Halmashauri hivyo Ilemela hakikisheni mnajiridhisha  na  makampuni ya kupima , uwezo wake, mpango kazi wake,pamoja na kuhakiki kama  michoro imezingatia maeneo ya huduma za jamii”, alihimiza CPA Makalla.


Aidha amewataka wataalam mhakiki madeni yote yanayohusiana na fidia za ardhi kwa watu waliotoa ardhi yao katika taasisi za serikali, wanaodai fidia katika mpango wa Kupima kupanga na kumilikisha (KKK) wanaodai fidia kupisha ujenzi au miundombinu yote yaainishwe yanayotokana na ardhi .


“Mstahiki Meya uwatake wataalam kuhakiki madeni yote ya ardhi kwani huwezi kutatua tatizo kama hujui ukubwa wa tatizo, ukishajua ukubwa wa tatizo utaweka mipango ya muda mfupi wa kati na mrefu katika kutatua matatizo” alisema CPA.Makalla


Nae mstahiki meya Mhe. Renatus Mulunga amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuendesha zoezi hilo la kusikiliza kero za wananchi huku akimuahidi  ushirikiano sambamba na kutekeleza na kuyafanyia maelekezo kuyafanyia kazi ambapo amewataka watendaji kutimiza wajibu wao.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.