• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC MAKALLA ASISITIZA NIDHAMU KWA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: June 1st, 2023

Watumishi wametakiwa kuwa na nidhamu katika kufanya kazi pamoja na kuhakikisha wanatoa huduma bora ili kuepusha chuki kati ya wananchi na Serikali yao itakayosabababishwa na utendaji kazi mbovu


Rai hiyo imetolewa  na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Gabriel Makalla alipofika kujitambulisha kufuatia kuhamishiwa kwake na Mhe. Rais Mkoani Mwanza mapema mwezi huu.


"Mkiwahudumia vyema mwananchi wataipenda Serikali na kinyume chake wataichukia hivyo tuepushe migogoro na migongano kwenye maeneo yenu ya kutolea huduma.Ipende kazi yako, timiza wajibu wako" CPA Makalla.

Sambamba na hilo CPA Makalla amewataka viongozi wa wilaya ya Ilemela kusimamia masuala ya Usalama wa jamii ili wananchi wawe huru kufanya kazi za kujitafutia maendeleo na kusisitiza kuwa suala la usalama ni kipaumbele chake


"Watu wakikosa usalama watakosa amani ya kufanya mambo ya Maendeleo hivyo lazima tukumbushane umuhimu wa kuwa na amani kwenye maeneo yetu ili kuleta tumaini kwa wananchi kuwa wapo huru kujitafutia kipato." Amesema Makalla.


Vilevile, ameiagiza Halmashauri hiyo kusimamia kwa dhati ukusanyaji wa mapato ya ndani ili wawe na rasilimali za kutosha kutekeleza miradi mbalimbali kwa jamii na kwamba wote kwa pamoja ni lazima wadhibiti Mapato ya ndani na wajiwekee utaratibu wa kujibu Hoja za Ukaguzi kwa wakati.


"Hakikisheni fedha zote zinazokusanywa zinakwenda Benki ili tuweze kujihakikishia ukusanyaji mzuri na  kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza miradi mbalimbali na wabadhirifu wa fedha wajue kabisa kuwa tunawafuatilia" Amesisitiza.


Nae Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Masala akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Wilaya ya Ilemela kwa Mkuu wa Mkoa, alisema kuwa wilaya ya Ilemela inaendelea kuboresha mazingira kwa kuwaletea huduma bora za Miundombinu, Elimu na Afya na kwamba makundi yote yanawezeshwa vema kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii.


Huku akibainisha kuwa kwa Mwaka wa fedha unaoendelelea (2022/23) Manispaa ya Ilemela ilikadiria kukusanya Shilingi Bilioni 13 na hadi sasa wamekusanya zaidi ya bilioni 14 ambayo ni sawa na asilimia 109 na wanaendelea kutekeleza Miradi yenye thamani ya Bilioni 18.


Akitoa neno la Shukran Naibu Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe Manusura Sadiki amemuomba kusaidia upatikanaji wa mabasi yatakayoanzia safari zake katika kituo kikuu cha malori na mabasi Nyamhongolo ili kuongeza thamani ya fedha zaidi ya bilioni 24.6 zilizotolewa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hasan kujenga kituo hicho pamoja na kumhakikishia ushirikiano wa viongozi wa wilaya hiyo katika kuwatumikia wananchi



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.